
Naibu Waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya amewahimiza wazazi wenye watoto walio na mtindio wa ubongo kuwapeleka watoto wao shule ili wakapate elimu huku akiwaonya wasiowapeleka watachukuliwa hatua za kisheria.

Ameyasema hayo leo alipokuwa katika ziara ya Shule maalum ya Msingi Sinza na kujionea hali halisi ya kielimu ya wanafunzi wenye mtindio wa ubongo.

Amesema wazazi wanapaswa kuthamini hasa watoto wenye mahitaji maalum kama walivyo watoto wengine wanaoanza shule kwa wakati mwafaka kiumri.

Pia amejionea baadhi ya changamoto zilizopo katika shule hiyo na kuahidi kuzifanyia kazi huku akianza kwa kutoa pesa kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya kutengeneza bembea zilizoharibika kwa ajili ya michezo ya wanafunzi hao.

NA DENIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS

