The House of Favourite Newspapers

Mapya Kifo cha Mke wa Mzee Yusuf.. Leilah, Khadija Yusuf Wachefua Ndugu!

0
Khadija Yusuf (aliyefumba macho kulia)

 DAR ES SALAAM: Siku chache tu tangu kufariki dunia kwa mke wa pili wa aliyekuwa Mfalme wa Taarab Bongo, Alhaj Mzee Yusuf aitwaye Chiku Khamis, mapya yameibu­ka huku dada wa mume na mke mkubwa, wakiwachefua wanandugu, Risasi lina habari kamili.

Mwili wa Chiku na kichanga chake ulizikwa Jumapili iliyopita katika Makaburi ya Kisutu am­bapo kabla ya kuzikwa uliagwa nyumbani kwa wazazi wake Mtaa wa Livingstone, Kariakoo ambako kuliibuka mambo ya kushangaza.

NYUMBANI KWA WAZAZI WA MAREHEMU

Chanzo makini ambacho ki­likuwa msibani hapo kilieleza kuwa, mke wa kwanza wa Mzee Yusuf ambaye pia ni mwimbaji wa Taarab katika Kundi la Ja­hazi Modern, Leilah Rashid na wifi yake, Khadija Yusuf walizua minong’ono baada ya wifi huyo kukataa kupokea mkono wa pole.

“Unajua pale msibani ndugu wa Chiku na wa Mzee Yusuf, yaani mama yake na dada zake wa­likuwa karibukaribu hivyo baada ya mwili wa marehemu kupelekwa makaburini, watu wakawa wana­toa mkono wa pole.

“Cha kushangaza Khadija al­ivyoona wifi yake Leilah anakwen­da kumshika mkono, akajifunika na juba lake usoni na hata alipotik­iswa na kumpa mkono, aliukataa ikabidi aendelee na watu wengine kuwashika mikono hali ambayo il­iwashangaza waombolezaji wengi walioshuhudia tukio hilo,” kilisema chanzo hicho.

Mzee Yusuf na mkee Leilah Rashid katika pozi la nyumbani

VIKAO VYAWEKWA KUWAJADILI

Chanzo hicho kiliendelea kutir­irika kuwa kutokana na tukio hilo la Khadija kukataa kupokea mko­no wa wifi yake, familia iliweka kikao na kujadili kwani lilionesha picha mbaya kwa watu.

“Familia ya Mzee Yusuf ilikerwa sana na tukio hilo ambapo iliweka kikao na kujadili kwa kina nini ki­fanyike lakini mpaka sasa muafa­ka waliofikia bado haujajulikana,” kilisema chanzo.

UTATA CHANZO CHA KIFO WAIBUKA

Bado utata ni mkubwa kuhusu chanzo cha kifo cha Chiku aliye­fariki dunia baada ya kufanyiwa upasuaji wa kujifungua ambapo Mzee Yusuf alisema baada ya kumfikisha katika Hospitali ya Amana, aliambiwa asubiri kidogo kwani wataalamu hawakuwepo kwa muda huo.

Leilah akiwa kwenye moja ya maonesho yake ya taarab

“Tulifika Amana wakati tu­nasubiri madaktari, Chiku akani­ambia anahisi kama chupa im­epasuka lakini kumbe ni damu zilikuwa zinamtoka.

“Wakati wa watu kuondoka wodini ulipofika tukatolewa nje na manesi wakaniambia ndiyo anapelekwa chumba cha up­asuaji kutokana na kuanza ku­vuja damu hivyo tukaondoka na kwenda kuzungukazunguka.

“Baadaye nikarudi ambapo niliitwa na daktari na kuniambia wamehangaika kuokoa maisha ya mtoto lakini hawakufanikiwa kwa sababu kondo lilikuwa lime­shapasuka, pia mama yake ali­fanyiwa upasuaji na kuamka vi­zuri na kuzungumza lakini baada ya dakika chache hali ilibadilika naye akafariki dunia.

“Nakumbuka maneno yake ya mwisho wakati ninambeba kumpeleka wodini alikuwa aki­niambia pumzi zinakata nikawa namwambia aendelee kusali na kutaja jina la Allah yaani naumia sana ila naomba Mungu anipe subira na naomba watu wani­ombee subira katika kipindi hiki kigumu,” alisema Mzee Yusuf.

Mmoja wa waombolezaji akilia kwa uchungu msibani.

WASINDIKIZAJI WENGINE NAO

Baadhi ya watu waliokwen­da pamoja na Chiku hospitalini hapo, walisema wakiwa chumba cha uzazi (Leba) walikaa muda mrefu kabla ya marehemu kuan­za kuhudumiwa, kitu ambacho wanaamini kilichangia kifo chake.

“Tulikaa sana kwa kweli, maa­na mara wakasema hawawezi kumhudumia tumpeleke Muhim­bili, mara wakasema tusubiri hadi hali yake ikaanza kuwa mbaya, hatujui mambo ya Mungu, lakini nadhani angewahishwa, angeti­biwa mapema,” alisema mtu huyo na kukataa kutajwa jina.

Mzee Yusuf na aliyekuwa mkewe Chiku Hamis, enzi za uhai wake

HUYU HAPA DOKTA AMANA

Risasi Mchanganyiko baada ya kufika Hospitali ya Amana na kushindwa kumuona Daktari Mkuu, kwa maelezo kuwa lina­paswa kuanzia kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, ambako nako kiongozi huyo hakuwepo ofisini, lilifanikiwa kuzungumza kwa njia ya simu ya ofisini hos­pitalini hapo na mtu al iyej i tambul isha kama Daktari Mkuu wa Amana.

“Siwezi kuku­jibu lolote hapa hadi nijue aliku­ja hapa aki­tokea hospitali gani, maana hapa ni hos­pitali ya rufaa, huenda wao ( h o s p i t a l i aliyotibiwa awali) ndiyo w a n a j u a zaidi tatizo lilikuwa ni nini na huenda ndicho kilichosababisha kifo chake, huwezi kusema ali­cheleweshwa kuhudumiwa bila kupata maelezo hayo,” alisema daktari huyo baada ya kuelezwa kuwa kucheleweshwa kuhudumiwa ndiko kulikosababisha kifo hicho.

MZEE YUSUF APEWA JUKUMU

Kutokana na yaliyo­jitokeza msibani, ya dada Khadija kukataa kushikwa mkono na mke wa kaka yake huyo, Leilah wadau mbalimbali wamempa ju­kumu la kushughulikia tatizo hilo ili liishe.

“Huu ni wakati muafaka wa Mzee Yusuf kuwapatanisha mkewe na dada yake maana kifo humaliza tofauti hivyo atum­ie kipindi hiki kumaliza bifu la wawili hao kwani ni muda mrefu hawapendani wala hawaongei,” alisema mmoja wa wadau.

TUJIKUMBUSHE

Leilah na Khadija ni mahasimu wa muda mrefu ambapo kila mmoja amekuwa mgumu kuwe­ka wazi chanzo cha bifu lao.

GLADNESS MALLYA | RISASI MCHANGANYIKO

 

INASIKITISHA! Tazama Mazishi ya Mke wa Mzee Yusuf na Alichokisema Makaburini

Leave A Reply