Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ametangaza kuwaita marais wa nchi tano za Ukanda wa Sahel, Desemba 16, 2019 katika mji wa Pau Kusini mwa nchi hiyo.
Macron amewaita marais wa Mali, Burkina Faso, Niger, na Chad kwenda kujieleza kufuatia vifo vya wanajeshi 13 wa Ufaransa vilivyotokea nchini Mali, Novemba 26, mwaka huu baada ya helikopta zao kugongana.
Aidha, Macron amesema ataondoa majeshi ya Ufaransa ndani ya nchi ambayo haitatoa maelezo ya kuridhisha.