Marekani: Waathirika wa Corona Virus Wafikia 104,256
MAREKANI imeendelea kuongoza kwa idadi kubwa ya kasi ya maambukizi ya virusi vya corona ambapo wamefikia 104,256 na waliopona ni 2,525 huku waliofariki wakiwa ni 1,704.
Italia ni ya pili ina wagonjwa 86,498, wamepona 10,950 na waliofariki ni 9,134.
Maambukizi yanapungua China ambayo ni ya tatu ikiwa na wagonjwa 81,394, walipona 74,971 na waliofariki 3,295.