RAIS wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema kuwa mashambulio yanayofanywa na Urusi yanalenga maeneo muhimu yanayozalisha umeme hali inayosababisha kukosekana kwa nishati hiyo muhimu.
Kutokupatikana kwa umeme Ukraine kumesababisha takribani mamilioni ya wakazi wa nchi hiyo kuathirika kwa nishati hiyo.
Meya wa Kharkiv Ihor Terekhov alisema mashambulizi ya Urusi dhidi ya miundombinu ya raia yaliacha sehemu kubwa ya jiji lake bila umeme na maji Jumapili jioni. Aliliita jaribio hilo baya na la kijinga la kulipiza kisasi.
Terekhov na Gavana wa eneo hilo walitoa wito wa utulivu, wakisema huduma za dharura zinafanya kazi ya kurekebisha uharibifu na kuzima moto.
Imeandikwa: Leocardia Charles kwa msaada wa mitandao.