Maskini Mtoto Huyu! Miaka 8 Anatembelea Tumbo – Video
Binti Warda mwenye umri wa miaka 8 anaetembea kwa kutumia tumbo, si kwa kupenda yeye bali hana uwezo wa kusimama wala kutembea, si hivyo, Warda hawezi hata kuongea.
Alizaliwa akiwa mzima wa afya lakini alipofikisha umri wa miezi 6 akaugua degedege hali iliyomsababishia matatizo yote haya.
Warda anaishi na bibi yake ambaye hana uwezo wa kumtunza mtoto huyo kutokana na kipato chake kuwa duni.
Unaweza kumchangia chochote ili aweze kupatiwa matibabu na mazoezi ya mwili hatimae arudi katika hali yake ya kawaida. Namba 0738716524
Comments are closed.