The House of Favourite Newspapers

Mastaa 10 Wadaiwa Kuanika Miili Yao Kunasa Wanaume!

13556805_641387202683056_668619570_n

Gift Stanford ‘Gigy Money’

Hali ngumu na raha ya ubuyu usimung’unye mwenyewe! Ishu inayotrendi kwa sasa kwenye ulimwengu wa ubuyu wa mjini ni aibu ya baadhi ya mastaa wa kike Bongo kudaiwa kuwanasa wanaume mtandaoni kwa njia ya picha zinazoonesha sehemu kubwa ya miili yao.

lulu-1

Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Kufuatia ishu hiyo, kumeibuka malalamiko kwamba, picha hizo haziishii tu mitandaoni bali zinawafikia hata watoto wao na kumomonyoa maadili ya Kitanzania kwani baadhi ya watu, wakishavutiwa nazo, huzichukua na kutumiana kwenye simu hivyo kusambaa kwa watu wengi zaidi.

Chanzo makini ambacho ni mfuatiliaji wa karibu wa ishu za mastaa kimeeleza kwamba, baadhi ya mastaa hao wamekuwa wakisingizia kuwa wanatangaza nguo hasa za ndani ndiyo maana huvaa kihasara.

gigy_money

Gigy Money.

UGUMU WA MAISHA?
Lakini nyuma ya pazia, inadaiwa kuwa kutokana na ugumu wa maisha kwa sasa, ndiyo mbinu mpya ya kujipiga promo kwa ajili ya kujiuza kwa wanaume ambao huwatafuta baada ya kuona picha hizo. “Ninyi hamjui tu! Kama hamuamini, chunguzeni, wasichana kibao wa mjini pamoja na baadhi ya mastaa wamebuni njia rahisi ya kujiuza mitandaoni. “Wanachokifanya ni kwenda studio na kupiga picha kali zinazoonesha maungo yao kisha wanatupia mitandaoni.

WAWILI WATANGAZA MAFANIKIO
“Kuna wawili (mastaa) ambao ni marafiki zangu, wanasema wamefanikiwa kupata dau kubwa kwa siku kutoka kwa wanaume kwa sababu tu ya kujipigia promo wenyewe,” kilimwaga ubuyu chanzo hicho.

amberlulu

Amber Lulu

WALIOTAJWA HAWA HAPA
Baadhi ya mastaa wanaotajwa kujipigia promo kwa wanaume ni pamoja na Isabela Mpanda ‘Bella’, Hamisa Mobeto, Gift Stanford ‘Gigy Money’, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Husna Maulid, Faiza Ally Lulu Semagongo ‘Aunt Lulu’, Mwanaisha Said ‘Dyna’ na Tunda Sebastian.

 

 

mobeto

Hamisa Mobeto.

UBUYU YABAINI KITU
Kufuatia sakata hilo, Kona ya Ubuyu Ulionyooka ilizungumza na baadhi ya mastaa waliotajwa ambapo wapo waliokiri kuwa, biashara hiyo inalipa zaidi kwani haina gharama lakini pia walidai kuwa kila mtu ana maisha yake na anajua anapopatia mkate wake wa siku bila kujali kujiondolea utu.

tunda-211

Tunda Sebastian.

MSIKIE GIGY:

“Kama inalipa, haimhusu mtu, ninachojua ni kweli wapo wanawake wengi wanaojiuza, cha muhimu ni kujua dau lako na siyo kufuatilia maisha ya wengine, mimi naishi maisha yangu.

” HUYU HAPA BELLA
Kwa upande wake Bella alifunguka kuwa, yeye si wale waliopo kwenye kundi hilo ila anapenda tu kupiga picha hizo kwa sababu ya mwili alionao na pia ikumbukwe kuwa aliwahi kuwa miss na kazi yake ya muziki na uigizaji vinamruhusu.

lul-an

Aunt Lulu.

TUNDA ANAFUNGUKA:
“Mimi napenda kufanya nitakacho, siangalii watu wanataka nini ILIMRADI ni ukurasa wangu, siwezi kuzuiwa kufanya lolote. Kuhusu wanaume, hata wakija wengi huwa nawapotezea tu na wala hawajakosea kwa sababu wapo wanaodhani tunapiga picha kwa ajili hiyo na kutuma komenti kibao.” Hao ni baadhi ya mastaa waliopatikana na kupewa nafasi ya kujitetea lakini katika uchunguzi wa Wikienda, ilibainika kuwa wengi wanaoweka picha hizo, lengo lao huwa ni kutangaza nguo kama walivyowahi kujitetea Hamisa Mobeto, Lulu na wengineo.

NENO LA MHARIRI
Siyo hukumu ya Wikienda wala msomaji wake kuwa mastaa wanaotajwa ni kweli kwamba wanajiuza kwa njia hiyo lakini kama kweli wanafanya hivyo, wanapaswa kujiheshimu kabla ya kuumbuliwa kwani kila mmoja anajua kwamba tukimvalia njuga tutamuumbua.

Kama ni suala la matangazo ya nguo, basi wafanye matangazo kwa wakati kisha kujiweka kiheshima na siyo kila nukta kutupia picha za nusu utupu. Pia kama ishu ni kukosa wachumba, wakumbuke kuwa ndani ya mitandao hiyohiyo kuna uwezekano wa kuwepo kwa wachumba na wakwe hivyo ni rahisi kupoteza sifa za mke bora.

Comments are closed.