The House of Favourite Newspapers

Mastaa Hawa Wamefunikana Kwelikweli Kwenye Ligi

0

TAYARI kivumbi cha Ligi Kuu Tanzania Bara kimeanza ambapo timu nyingi kwa sasa zimeanza kusaka pointi tatu ndani ya uwanja kwa msimu wa 2020/21.

Mabingwa watetezi ni Simba, walitwaa taji hilo msimu wa 2019/20 baada ya kucheza mechi 38 na kujiwekea kibindoni pointi 88.

Tayari Septemba 6 walikiwasha huku na watani zao wa jadi Yanga nao walikiwasha pia.Simba wao walikuwa Uwanja wa Sokoine kumenyana na Ihefu ambapo ilishinda mabao 2-1, Yanga wao walijiwekea ngome pale Uwanja wa Mkapa na ilitoshana nguvu kwa safari yake imeanza ndani ya Uwanja wa Sokoine na ana kazi ya kukiongoza kikosi chake kutetea taji la Ligi Kuu Bara.

 

Bocco aliyeyusha dakika zote 90 na alikiri kwamba Ihefu FC sio timu ya mchezomchezo ndani ya ligi licha ya kwamba ni msimu wake wa kwanza.

JOASH ONYANGO

Licha ya kwamba hakuwa na chaguo wakati akishuhudia shuti la Omary Mponda likizama ndani ya nyavu za kipa wake Aishi Manula, Onyango alipambana.

 

Kazi kubwa ilikuwa ni kuokoa hatari za Jordan John ambaye alikuwa ni msumbufu kwenye kambi yake aliweza kuokoa hatari mbili zilizokuwa zinakwenda langoni mwake.

 

Ameanza kujenga maelewano mazuri na mzawa, Kened Juma ambaye alikuwa kwenye kiwango bora mbele ya mabao yote mawili ya Simba, Uwanja wa Sokoine.

 

Alitoa pasi ya bao kwa nahodha John Bocco na alimaliza kazi aliyoianzisha yeye mwenyewe ya kupiga faulo aliyompa Clatous Chama, kisha Chama akammegea pande la pasi iliyojazwa kimiani na ‘bichwa’ lake na kuwafanya Simba wasepe na pointi tatu mazima.

Mechi yake ya kwanza ya msimu wa 2019/20 wakati Simba ikishinda mabao 3-1 mbele ya JKT Tanzania alihusika kwenye mabao mawili ambapo yote alitoa pasi Uwanja wa Uhuru ila msimu huu amefunga bao moja.

CLATOUS CHAMA

Ameanza kasi ya kuifukuzia rekodi yake ya utulivu Uwanja wa Mkapa, Septemba 6 huenda angesepa na mpira wake wa kwanza kwa kufunga ‘hat trick’ kwa kuwa alikosa nafasi nne ambazo mashabiki walikuwa wanahesabu kuwa ni mabao.

 

Alianza kwa kusepa na kijiji chake dakika ya 65 aliachia shuti ambalo lilitoka nje kidogo ya lango na dakika ya 80 alipiga shuti kali lilikweda nje kidogo ya lango. Akitumia dakika 45 alisababisha kona nne na alitoa jumla ya pasi 18.

MICHAEL SARPONG

Aliweza kutumia dakika 12 kuweka usawa ndani ya uwanja baada ya Lambart Charlse kuwatungua dakika ya 7 ambapo yeye aliweka usawa dakika ya 19 kwa shuti kali ndani ya 18 lilimshinda mlinda mlango wa Prisons, Jeremia Kisubi.kufungana bao 1-1 na Tanzania Prisons.

 

Championi Jumatano linakuletea namna nyota wa miamba hiyo miwili walivyokinukisha ndani ya uwanja hawa ni nyota wa Simba:-

 

BERNARD MORRISON

Amekabidhiwa jukumu la kupiga mipira iliyokufa ndani ya Simba. Alitumia dakika 67 uwanjani. Aliweza kuingia ndani ya box mara 10 na alisababisha kona moja na alipiga kona tatu ndani ya Simba.

 

Makeke yake Uwanja wa Sokoine kwa nyota huyo mwenye mabao mawili na pasi moja yaliwekwa mfukoni na safu ya mabeki wa Ihefu iliyokuwa chini ya Omary Kindamba aliyekuwa ni mtibua mipango namba moja kwa Simba.

MZAMIRU YASSIN

Mzawa huyu ndiye nyota wa mchezo kwa kuwa aliweza kuhusika kwenye Ihefu.Hawa wababe wa Yanga mbele ya Tanzania Prisons

 

BAKARI MWAMNYETO

Vita mpya ya namba mbele ya Lamine Moro hasa kwa nafasi ya beki wa kati imempata mtu anayejituma na kutimiza majukumu yake ndani ya uwanja.

 

Licha ya kuruhusu kutunguliwa bao moja na Tanzania Prisons dakika ya 7, lilimshtua beki huyu kutoka Coastal Union na kumfanya aongeze umakini na kutoa maelekezo kwa wachezaji wenzake.

 

Kipindi cha kwanza ambapo Tanzania Prisons walikuwa wa moto, Mwamnyeto aliweza kuituliza timu. Aliweza kutoa jumla ya pasi 27 katika harakati zake za kuweka lango lake salama na alikokota mipira mara sita ikiwa inaonyesha kwamba ana uwezo mkubwa wa kujiamini katika kazi yake.

 

TUISILA KISINDA

Kisinda alianza kuusoma kwanza mchezo wakati akisugua benchi ambapo aliingia dakika ya 45 akipishana na muziki wa kazi Deus Kaseke ambaye ni nahodha na kitambaa alikabidhiwa beki Abdalah Shaibu,’Ninja’,Kisinda angekuwa na pasi 10 na mabao mawili aliyofunga msimu uliopita wa 2019/20 kati ya mabao 78.

 

Ameweza kutaka tena Uwanja wa Sokoine ambapo msimu uliopita kwenye pasi zake 10 ni huo tu wa mkoani aliweza kutoa pasi ni wakati Simba ikishinda mabao 2-0 mbele ya Mbeya City.Aliweza kuziyeyusha dakika zote 90 huku akicheza kwa utulivu mkubwa ndani ya uwanja.

JOHN BOCCO

Kapten mzawa mwenye juhudi ndani ya uwanja aliweza kuonyesha uwezo wake kwenye mchezo wake wa kwanza mbele ya Ihefu ambapo ilimchukua dakika 10 kufungua akaunti yake ya mabao ndani ya ligi.

 

Msimu uliopita aliweza kufunga mabao 9 hivyo Ni bao lake la pili Uwanja wa Mkapa ambapo alianza kuwatungua Aigle Noir kwenye mchezo wa kitaifa wa kirafi ki Uwanja wa Mkapa, Septemba 30.Aliingia ndani ya 18 mara 11, alipiga jumla ya pasi 26,alichezewa faulo mara mbili.Nyota huyu ni ingizo jipya kutoka Rayorn Sport ya Rwanda na ni raia wa Ghana.

KIBWANA SHOMARI

Mzawa huyu aliyekuwa anakipiga ndani ya Klabu ya Mtibwa Sugar ameanza kumkalisha benchi rafi kiye Paul Godfrey ambaye wanacheza naye nafasi moja.Shomari ana uwezo wa kupiga mashuti nje ya 18 na mzuri kwa kumwaga maji ya uchonganishi kwa wachezaji ndani ya timu.Aliyeyusha dakika zote 90 na ana jukumu la kupiga kona pia ndani ya Yanga hivyo akishazoea mfumo atafanya mengi kwa wana Jangwani.

 

YACOUBA SOGNE

Ingizo jipya kutoka Asante Kontoko ya Ghana, raia huyu wa Burundi aliweza kuonyesha makeke yake kwa muda wa dakika 45 akipishana na jembe la kazi Farid Mussa ambaye aliwasumbua Prisons kipindi cha kwanza.Yacouba alisababisha kona nne na alitoa jumla ya pasi 16 alionyesha uwezo wa kukokota mpira mara mbili na alicheza faulo ya kizembe mo

Leave A Reply