MASTAA WALIOKUMBANA NA MIFADHAIKO YA AKILI
PAMOJA na mafanikio waliyo nayo mastaa wengi, bado huwa wana matatizo na mifadhaiko ya kimawazo au kiakili. Kwa vile watu hao wanafahamika zaidi, si rahisi kujificha. Baadhi yao wakiwemo Demi Lovato, Catherine Zeta-Jones, na Jon Hamm, wameeleza changamoto walizokutana nazo hapo nyuma kuhusu hali hiyo.
Michelle Williams
Mwimbaji huyo wa zamani wa kundi la Destiny’s Child amesema aliwahi kutafuta ushauri kuhusu mifadhaiko ya akili na anakiri aliweza kusaidiwa na wataalam wa masuala hayo na kurejea katika hali njema.
Janet Jackson
Mwimbaji huyo maarufu anasema aliwahi kukumbwa na mfadhaiko lakini sasa yuko vyema baada ya kupitia katika furaha na misukosuko kibao.
Kanye West
Aliwahi kukumbwa na mfadhaiko wa akili, hata hivyo anasema yote hayo yamepita, yuko sawa na nguvu kubwa.
Mariah Carey
Mwimbaji huyo aligundulika kuwa na mfadhaiko wa akili mwaka 2001 lakini anasema “hivi sasa niko sawa kabisa”.
Mel Gibson
Anakiri kukumbana na mfadhaiko wa akili mnamo mwaka 2011 na anasema hayo ndiyo maisha ambayo watu wengi huyapitia.
Comments are closed.