MASTAA WAMPONGEZA SHEMEJI YAO UCHEBE!
MASTAA wa filamu Bongo, Jacob Steven ‘JB’, Steven Mengele ‘Nyerere’ na Single Mtambalike ‘Richie’ wamempongeza shemeji yao, mume wa msanii mwenzao Zuwena Mohammed ‘Shilole’, Ashiraf Uchebe kwa kumbadili na kumuweka kwenye maadili ya kidini tofauti na alivyokuwa zamani.
Jambo hilo la kumpongeza Uchebe lilichukua nafasi kwenye msiba wa msanii mwenzao Salome Nonge ‘Mama Abdul’ baada ya Shilole kuonekana kubadilika sana kwani hata mmoja wa wasanii alipommwagia pombe kwa bahati mbaya, alionesha kumaindi kuliko maelezo.
“Jamani Uchebe hongera sana maana kazi uliyofanya sio ndogo, nakuambia ni kazi kubwa. Yaani dada yetu Shilole leo hii anaona pombe anaruka hivi? Shemeji yetu hongera, umetukosha,” alisema Nyerere huku wote kwa pamoja wakiinuka kwenda kumpa mkoko Uchebe.
Comments are closed.