Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetaja wanafunzi 10 bora kitaifa waliofanya vizuri katika matokeo ya kuhitimu elimu ya msingi, ambapo wanafunzi sita kati ya 10 wanatokea shule za kanda ya ziwa.
Dk Msonde amewtaja watahiniwa 10 bora kitaifa na shule zao kwenye mabano ni Ndemezo Lubonankebe (Kadama-Geita), Innocent Seleli (Carmel-Morogoro), Given Malyango (Tumaini Junior –Arusha), Diomedes Mbogo (St Achileus Kiwanuka-Kagera), Sweetbert John (Mingas-Shinyanga).
Najma Manji (Nyamuge-Mwanza), Beatrice Jeremiah (Mapinduzi B-Mara), Mohamed Abdirahman Mohamed na Luqman Ally (Raskazone-Tanga) na Francisco Maiga (Kadama-Geita).
Comments are closed.