The House of Favourite Newspapers

Matokeo Kidato cha Nne: Wanafunzi 10 Bora Kitaifa, Shule 10 Bora

0

 

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) nchini Tanzania limetangaza matokeo kidato cha nne 2019 yakionyesha watahiniwa 340,914 sawa na asilimia 80.65 ya watahiniwa 422,722 wamefaulu mitihani yao.

 

Matokeo hayo yametangazwa leo Alhamisi, Januari 9, 2020 na Katibu Mtendaji wa Necta, DkT. Charles Msonde ambapo amesema watahiniwa hao ni sawa na ongezeko la asilimia 1.38 ikilinganishwa na watahiniwa 284,126 sawa na asilimia 79.27 waliofaulu mtihani huo mwaka 2018.

 

Katika matokeo hayo, Dk Msonde ametangaza wanafunzi 10 bora kitaifa ambapo kati yao sita wanatoka Shule ya Sekondari Francis Girls ya jijini Mbeya. Wanafunzi hao ni;

 

  1. Joan Ritte (St Francis Girls- Mbeya)
  2. Denis Kinyange (Nyengezi Seminary- Mwanza)
  3. Erick Mutasingwa (Sengerema Seminary- Mwanza).
  4. Rosalia Mwidege (St Francis Girls-Mbeya)
  5. Domina Wamara (St Francis Girls-Mbeya)
  6. Mvano Cobangoh (Feza Boy’s- Dar es Salaam)
  7. Agatha Mlelwa (St Francis Girls- Mbeya)
  8. Sarah Kaduma (St Francis Girls –Mbeya
  9. Shammah Kiunsi (St Francis Girls – Mbeya)
  10. Luck Magashi (Huruma Girls- Dodoma)

 

KUTAZAMA MATOKEO HAYO LINK ZIPO HAPA CHINI

Breaking: Matokeo Kidato cha Nne Yatangazwa, Haya Hapa

Breaking News: Matokeo Kidato cha Pili, Haya Hapa

Breaking: Matokeo Darasa la Nne Yatangazwa, Yasome Hapa

Leave A Reply