Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Lupita Nyong’o Asherehekea Ushindi wa Baba Yake
MWIGIZAJI aliyeshinda tuzo ya Oscar Lupita Nyong’o leo Agosti 11, 2022 amempongeza baba yake kwa kushinda muhula wa pili na wa mwisho kama gavana wa kaunti ya Kisumu nchini Kenya.
Baba yake, Anyang Nyong’o, alitangazwa mshindi Jumatano baada ya kura za uchaguzi mkuu wa Kenya siku ya Jumanne.
Muigizaji huyo aliyeshinda tuzo ya Oscar alilelewa nchini Kenya, kabla ya kuhamia Marekani.
Nyong’o, ambaye alishinda mwigizaji bora msaidizi kwenye tuzo za Oscar kutokana na filamu iitwayo 12 Years a Slave, aliwashukuru watu wa Kisumu kwa “msaada wao mkubwa” kwa baba yake kwenye uchaguzi.
ABICH MORO! Congratulations to my Daddy and THANK YOU to the people of Kisumu for their overwhelming support at the polls. @AnyangNyongo #5moro #TichTire pic.twitter.com/FEmgmGhB3j
— Lupita Nyong’o (@Lupita_Nyongo) August 10, 2022