Matukio Mbalimbali ya Msiba wa Filikunjombe
Mke wa marehemu Deogratius Filikunjombe, Sarah Filikunjombe (katikati) akifarijiwa.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayemaliza muda wake, Anne Makinda, akimfariji mke wa marehemu.
Anne Makinda akiwafariji wafiwa wakati mwili ulipoagwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe (kulia) akiteta jambo na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuber Kabwe wakati wa kuuga mwili wa Filikunjombe.
Mgombea urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimfariji mke wa marehemu, Sarah Filikunjombe wakati wa kuuaga mwili katika Hospitali ya Lugalo.
Miili ya marehemu waliofariki kwa ajali ya Helikopta ikiwa kwenye majeneza.
Viongozi wa kiserikali wakiwa msibani kuuaga mwili wa Filikunjombe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipowasili katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo kuwafariji wafiwa wakati wa kuuaga mwili wa Filikunjombe.
Huzuni, simanzi vikitawala wakati wa kuuaga mwili wa Filikunjombe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete akipita mbele kutoa heshima ya mwisho katika jeneza la Filikunjombe.
Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda akimfariji mke wa marehemu, Sarah Filikunjombe.
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ambeye pia alikuwa rafiki mkubwa wa marehemu akimfariji mke wa marehemu.
Watoto wa marehemu, Deogratius Filikunjombe (wakimkumbatia mama yao) nyumbani kwao wakati wa kuaga miili.
Waombolezaji wa eneo la Mtoni-Kijichi wakiwa katika hali ya simanzi nyumbani kwa marehemu, Filikunjombe.
NA DENIS MTIMA/GPL