The House of Favourite Newspapers

Matukio ya kufanya usafi yalivyokuwa Dar leo

0

1.Baadhi ya maduka yaliyopo maeneo ya mitaa ya Tandale yakiwa yamefungwa kutekeleza agizo lam Mkuu wa Mkoa wa Dar la kuwataka kufunga  nyakati za asubuhi kwa ajili ya usafi.

Baadhi ya maduka yaliyopo mitaa ya Tandale sokoni yakiwa yamefungwa kutekeleza agizo la mkuu wa mkoa wa Dar la kuwataka kufunga maduka yote asubuhi ili usafi ufanyike.

2.Wakazi wa maeneo ya Tandale wakifanya usafi kwenye maeneo yao hii leo Desemba 9, 2015.

3.Harakati za hapa na pale za kufanya usafi mitaa ya tandale ikiendelea.

Wakazi wa maeneo ya Tandale Sokoni wakifanya usafi.

4.Wakazi wa eneo la Mazese Darajani wakisafisha kwenye ngazi za kupanda juu ya daraja hilo.

Wakazi wa Manzese Darajani wakisafisha ngazi za daraja la wapita kwa mguu.

5.Wafanyakazi wa Bank ya Akiba Commercial Bank wakiungana na wananchi wa maeneo ya soko la Tandale kufanya usafi sokoni hapo.

Wafanyakazi wa Benki ya Akiba Commercial Bank wakiungana na wananchi wa Tandale Sokoni kufanya usafi .

6.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba (wakwanza kushoto) akiweka uchafu kwenye toroli la kubeba taka.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba Commercial Bank (ACB), Israel Chasosa (wa kwanza kushoto) akiweka uchafu kwenye toroli la taka.

7.Wafanyakazi wa Benk hiyo wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kufanya usafi.

Wafanyakazi wa ACB wakiwa kwenye picha baada ya kumaliza usafi.

8.Msanii wa Muziki wa Bongo fleva, Tunda man (katikati) akiwa na wasanii wenzake wakifanya usafi maeneo ya Tandale sokoni hii leo Desemba 9,2015.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Tundaman (katikati) akiwa na wasanii wenzake wakifanya usafi Tandale Sokoni.

9.Baadhi ya wakazi wa eneo la Tandale sokoni wakiwashudia wasanii hao kwenye zoezi hilo la  kuunga kampeni ya raisi Magufuli la kusafisa maeneo yao.

Wakazi wa Tandale wakiwashuhudia wasanii waliokuwa kwenye zoezi la usafi.

10.Maeneo ya manzese yakionekana kuwa safi baada ya zoezi la usafi kumalizika  nyakati za saa tano.

Maeneo ya Manzese ‘Tip Top’ yakionekana safi baada ya zoezi la usafi.

11.Barabara inayotoka Bamaga kuelekea Shekilango maeneo ya Sinza Afrika Sana mitaro ya maeneo hayo  ikionekana kuwa safi.

Hapa ni Sinza Afrika-Sana baada ya mitaro yake kusafishwa.

12.Wakazi wa eneo la Mbezi ya Kimara wakifanya usafi kuadhimisha siku ya Uhuru Desemba 9,2015 ikiwa moja ya kampeni ya kusafisha.

Wakazi wa Mbezi ya Kimara wakiongozwa na mwenyekiti wao wa mtaa wa ‘Mbezi kwa Yusufu’, Joseph Mbuya (kulia) wakisafisha eneo lao.

13.Akina mama wa eneo la stendi ya mbezi ya Kimara wakitumia kauli ya rais Maufuli ya 'Hapa Kazi Tu' kusafisha mazingira ya maeneo yao.

Kina mama wakishiriki usafishaji mazingira huko Mbezi-Kimara.

SHUGHULI ya kufanya usafi nchini ilipamba moto pia katika Jiji la Dar es Salaam kufuatia wito wa Rais Dk. John Magufuli wa kuitumia siku ya uhuru wa Tanzania Bara kwa ajili ya wananchi kusafisha mazingira sehemu za makazi na makazini mwao.
Kamera yetu leo ilitembelea maeneo mbalimbali ambako shughuli hiyo ilifanyika, miongoni mwake yakiwa ni Tandale Sokoni, Manzese Darajani, Mbezi ya Kimara.

PICHA / HABARI: DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply