Maua Sama: Bila Mwana FA nisingekuwa hapa
Mwanadada Maua Sama katika pozi tofauti ndani ya studio za Global TV Online leo kabla ya mahojiano.
Maua Sama akiwa na mtangazaji wa Global TV Online, Shorvieny Mohammed.
Maua akiwa na Mhariri wa Gazeti la Amani, Andrew Carlos.
Mhariri Msaidizi wa Gazeti la Ijumaa Wikienda, Gabriel Ng’osha akiwa na Maua.
Maua akila pozi na Walusanga Ndaki wa Global.
Maua na Mwandishi wa Championi, Nicodemus Jonas wakipata ‘selfie’.
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Maua Sama kwa mara ya kwanza amefungukia mafanikio yake kimuziki kwa kusema kuwa bila ya staa wa muziki wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ asingekuwa alipo saa.
Akizungumza katika kipindi cha Mtu Kati kinachorushwa na Global TV Online, Maua anayebamba na Ngoma ya Mahaba Niue alianza kwa kusimulia kwa jinsi alivyokutana na Mwana FA.
“Ilikuwa kitu cha ajabu kwangu. Wimbo wangu wa kwanza kabisa kuuimba ulikuwa So Crazy na kipindi nimeuimba nilikuwa chuoni Moshi, basi marafiki zangu wakamtumia wimbo huo MwanaFA bila mimi kujua na baada ya wiki nikashangaa kupigiwa simu na Mwana FA akaniambia amependa ninavyoimba na kwamba yupo tayari kuni-meneji na pia kunishirikisha,” alisema Maua.
Imeandaliwa na Andrew Carlos/GPL