The House of Favourite Newspapers

Maumivu ya Kiuno

MAKALA: UWAZI | AFYA

KIUNO kuuma ni tatizo la kiafya na ni moja ya mambo ambayo yanasaba­bisha idadi kubwa ya watu kwenda mahospitali eidha kulazwa au kuhudhuria kliniki kutibiwa.

Maumivu ya mgongo au kitaalamu lumbago yana uhu­siano mkubwa sana na misuli na mifupa. Ni vyema kwanza tukaangalia mfumo wa mgon­go wa mwanadamu ambao ki­taalamu huitwa vertebrae.

Sehemu ya juu eneo la shingo linaitwa cervical spine, sehemu ya mabega na chini yake hu­itwa thoracic na sehem ya chini ya mpaka makalio yanapoan­zia huitwa lumber. Ukishuka chini kidogo kuanzia makalio yanapoanzia seheme ya chini yenye mwonekano kama mkia huitwa coccyx.

Maumivu ya kiuno yanawe­za sababishwa na matatizo kwenye nyonga kitaalamu sac­roiliac au misuli hali ambayo huitwa lumbago.

Mifumo ya fahamu nayo haswa ya sciatica nerve (ei­dha neuralgia au neuritis) hali hii huanza kusikika pale am­bapo kutakuwa na kuguswa au kuathiriwa na kitu chochote. Hali hiyo husababisha mawasiliano kukatika kati ya ubongo na mig­uu na matokeo yake ni mtu kuwa mlemavu yaani kushindwa kun­yanyua mguu au kuusogeza.

VYANZO

Katika pingili yaani vertebral disc maumivu yanatokea pale ambapo kutakuwa na kupasu­ka au kulika kwa gegedu zina­zounda pingili za kiuno. Misuli dhaifu na tindikali nyingi inayo­ingia kwenye damu pamoja na upungufu wa madini ya chokaa hali huwa mbaya zaidi.

Kuharibika kwa misuli eneo husika, mifupa na kano kitaala­mu ligament, figo na kibofu cha mkojo, matatizo ya tezi dume au kizazi kwa akina mama ni sababu za mtu kuumwa mgongo.

Misuli iliojishikiza kwenye kiuno huathiriwa na tabia mbaya ya ulaji na uvaaji usiozingatia kanuni za afya bila kusahau ma­gonjwa ya mifupa yaani arthriti.

Mkao mbaya uathiri sana pin­gili za uti wa mgongo na hata kutembea ukiwa umepinda hii ni kwa wale wenye maringo.

Comments are closed.