The House of Favourite Newspapers

Mavoko Aibuka na Mapya ya Lulu Diva!

0

Dar: Msanii wa Bongo Fleva, Richard Martin ‘Rich Mavoko’ amesema siyo kweli kwamba ana uhusiano wa kimapenzi la mwenzake, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’.

 

Mavoko au Messi wa Bongo Fleva, ameliambia Gazeti la IJUMAA kuwa, ukaribu wake na Lulu Diva ndiyo ulisababisha watu kuanza kuzungumza hayo, lakini hakuna jambo kama hilo.

 

“Maisha yangu yamekuwa ‘private’ sana tangu nianze muziki ndiyo maana watu wanajua ni Lulu Diva kwa sababu nilikuwa naye karibu, lakini siyo mpenzi wangu, sipendi kuweka mapenzi yangu hadharani,” amesema Mavoko.

Stori: Imelda Mtema. Ijumaa

Leave A Reply