The House of Favourite Newspapers

Maxime: Mtibwa Kushuka Daraja ni Aibu Kubwa

0

NAHODHA na kocha wa zamani wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime amefunguka kuwa kama timu hiyo itashuka daraja, basi itakuwa ni aibu kubwa kwa kila mtu anayehusika na timu hiyo.

 

Maxime ambaye pia alikuwa kocha wa Kagera Sugar amesema aibu hiyo kubwa itamkumba hata yeye kwa sababu ndiye mchezaji pekee ambaye huenda alicheza timu hiyo kwa muda mrefu bila kuhama hadi anatundika daruga na kuhamia kwenye masuala ya ukocha.

 

Maxime alisema ukiitazama Mtibwa ina kila kitu, kuanzia wachezaji, makazi na hata kwenye masuala ya malipo siyo tatizo kubwa, hivyo timu kama hiyo ikashuka daraja inakuwa ni aibu kwa kila mtu.

 

“Mtibwa kushuka daraja ni aibu kubwa sana, kwa sababu ni kati ya timu ambayo ina wachezaji bora na ina kila kitu.

 

Mfano mtu kama mimi ndiyo nitaumia zaidi kwa sababu ndiyo timu yangu na nimecheza timu hiyo tu hadi nastaafu soka,” alisema.

STORI NA ISSA LIPONDA | CHAMPIONI JUMATATU, MEI 17, 2021

Leave A Reply