The House of Favourite Newspapers

Mbasha Amwaga Ubuyu wa Agness, Afunguka Kuoa – Video

MWIMBAJI wa Muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha amefunguka kuhusu uhusiano wake na msanii wa Modeling ambaye pia ni video queen, Agness ambaye miezi miwili iliyopita nyepesi zilisambaa kwamba wana uhusiano wa kimapenzi.

 

Akipiga stori na Global TV Online, Mbasha amesema uhusiano wake na Agness ni wa urafiki wa kawaida wala si wa kimapenzi. “Agness alivutiwa na kazi zangu uimbaji wa muziki wa Gospo, akawa shabiki yangu na rafiki yangu pia kupitia mitandaoni, sina uhusiano naye mwingine tofauti na urafiki wa kawaida,” alisema Mbasha.

 

Kuhusu kuoa mwanamke mwingine atakayeziba pengo la aliyekuwsa mkewe, Madam Flora, Mbasha amesema kwa sasa hana mpango wa kuoa kwani hajapata msichana wa kumuoa, labda baadaye endapo atapata mtu akavutiwa naye, basi hatasita kufanya hivyo.

Mbasha Amwaga Ubuyu wa Agness, Afunguka Kuoa – Video

Comments are closed.