The House of Favourite Newspapers

Mbowe na Wenzake Wawasili Polisi – Video

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe akitoka Sentro leo.

 

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na wenzanke wameripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es salaam leo ikiwa ni sehemu ya masharti ya dhamana waliopewa mahakamani katika kesi yao inayowakabili.

 

 

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Vicent Mashinji akitoka.

 

Mbowe na viongozi wenzake walifika polisi kwa nyakati tofauti leo asubuhi na kuonekana wakiingia katika ofisi hizo kwa muda kadhaa kisha baadaye wakatoka.

Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalim (kulia) akiongea na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Kata ya Vijibweni Ernest Mpuya, alipowasili Kituo cha Polisi.

 

Mbowe na wenzake ambao ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji na manaibu wake wa Bara na Zanzi­bar, John Mnyika na Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko, John heche na Halima Mdee wote wanakabiliwa na mashtaka manane yakiwemo mawili ya uchochezi wa uasi yanayom­kabili Mbowe.

Mwenyekiti wa BAWACHA, Halima Mdee (wa mbele ) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Ester Bulaya wakiwasili Kituo cha Polisi Kati Dar es salaam, leo Ijumaa.

Ndani ya makosa hayo, wanadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na uliopelekea maandamano na vurugu zilizosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini na askari polisi kujeruhiwa, Feb. 26.

Wabunge Peter Msigwa na John Heche wakitoka Kituo Kikuu cha Polisi kati Dar, walipotakiwa kuripoti ikiwa ni moja ya sharti la dhamana ya shauri namba 112/2018, leo Ijumaa Aprili 13, 2018.

Akizungumza baada ya kutoka kituoni hapo, Mashinji alismea;

“Mhe. Ester Bbulaya ataunganishwa kwenye shauri hili lakini kwa sasa amebaki kituoni kwa taratibu za kiupelelezi lakini tunafuatilia kwa ukaribu.”

Comments are closed.