The House of Favourite Newspapers

Mbunge Adai Kutekwa na Kuuawa ni Jambo la Kawaida

 

MBUNGE wa Singida Magharibi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Elibariki Kingu amedai kuwa vitendo vya watu kutekwa na kuuawa ni jambo la kawaida huku akilishauri Bunge kutounda Tume kuchunguza kwani itazua taharuki na Serikali haijashindwa kusimamia usalama wa nchi na raia wake.

 

Kingu amesema kuwa, matukio ya kihalifu yapo kila utawala na hakuna Taifa linaloweza kwenda bila ya kuwa na uhalifu.

Kauli yake inakuja wakati Taifa bado liko kwenye sintofahamu kuhusu kutekwa nyara kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake watatu, kupigwa risasi kwa Mbunge Tundu Lissu, Azory Gwanda, Ben Saanane, Salma Said na mauaji Alphonce Mawazo, Daniel John na Godfrey Lwena na mauaji ya wananchi wilayani Kibiti, Rufiji, Mkuranga- Pwani.

Kauli ya Kingu imekuja kama majibu kwa Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe aliyewasilisha kwa Katibu wa Bunge barua ya kusudio la kuwasilisha Hoja Binafsi ya kuunda Kamati Teule ya Bunge kuchunguza matukio mbalimbali yanayoonesha kutishia umoja, usalama na mshikamano wa Taifa letu.

 

ABDUL NONDO APATIKANA AKIWA HAI IRINGA, POLISI WAMCHUNGUZA!

Comments are closed.