The House of Favourite Newspapers

Mdogo wa Rais Afungwa Jela

0

Mdogo wa aliyekuwa rais wa Algeria hayati, Abdelaziz Bouteflika, amefungwa gerezani kwa kipindi cha miaka miwili kwa kosa la kukwamisha haki kutendeka.

 

Said Bouteflika alifungwa pamoja na waziri wa zamani wa haki, Tayeb Louh, pamoja na mfanyabiashara , Ali Haddad.

 

Louh atatumikia kifungo cha miaka sita wakati bwana Haddad atafungwa miaka miwili. Wote watatu walikamatwa baada ya rais Bouteflika alipoondolewa madarakani kwa lazima mnamo mwaka 2019. Rais wa zamani wa Algeria ,Bouteflika alifariki mwezi uliopita, miaka nane baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Leave A Reply