Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers, Eric Shigongo (wapili kulia) akimpa mkono wa pole Meneja wa Global, Abdallah Mrisho (mwenye shati nyeusi).
Kutoka kushoto ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers, Richard Manyota, Meneja, Abdallah Mrisho na Mkurugenzi Mtendaji, Eric Shigongo.
Mkurugenzi wa Global Publishers, Lydia James (katikati) akimpa pole Abdallah Mrisho (wa kwanza kulia), pembeni yake ni baadhi ya wafanyakazi wa Global.
Huzuni zikiwa zimetawala kwa waombolezaji msibani hapo.
Jeneza lenye mwili wa marehemu likishushwa kwenye gari kwa ajili ya kuswaliwa katika Msikiti wa Al-Imran Tabata-Makame.
Meneja wa Global, Abdallah Mrisho (aliyeko mbele) akiongozana na waombolezaji waliokuwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu, Dawood Mrisho kwa ajili ya kusafirishwa Mkoani Tabora.
Waombolezaji wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu kupeleka katika gari tayari kuelekea mkoani Tabora kwa mazishi.
Mdogo wa marehemu, Abdallah Mrisho (mwenye shati nyeusi) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa kaka yake.
Baadhi ya wafanyakazi wa Global (waliopo mbele) wakiungana na wakazi wa eneo la Tabata katika maombolezo.
Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu, Tabata-Makame jijini Dar.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Global Publishers, Abdallah Mrisho amepata pigo kwa kufiwa na kaka yake, Dawood Mrisho aliyefariki jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Global Publishers, wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Eric Shigongo wameungana na ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu katika maombolezo ya msiba huo, nyumbani kwa marehemu, Tabata-Makame.
Mwili wa marehemu umeagwa nyumbani hapo na kusafirishwa kijijini kwao Tarafa ya Bukene-Nzega Mkoani Tabora kwa ajili ya mazishi.
NA DENIS MTIMA/GPLA