The House of Favourite Newspapers

Meninah Ameacha Mambo ya Wasichana

MSANii wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa amejitosa kwenye uigizaji, Meninah amefunguka kuwa anajiona ameshakuwa mwanamke mkubwa hivyo mambo ya wasichana amewaachia wenyewe.

 

Meninah ameliambia Gazeti la ijumaa kuwa kuna kipindi huwa kinafika kwenye maisha kila kitu kinabadilika na mfumo mzima unabadilika na kuwa tofauti na ndivyo alivyo yeye hivi sasa.

 

“Nimekuwa mwanamke kamili hivyo mambo ya wasichana nimeyaweka pembeni, nasimama kama mama ninayejua baya na zuri maana kuna wakati ukifika lazima mtu ungalie lipi la kufanya na lipi la kuweka pembeni,” alisema Meninah.

Stori: Imelda Mtema, Dar

TFF Yashindwa ‘KUJIZUIA’ Yawajibu Wanaomsema Kocha AMUNIKE “Mnawakatisha Tamaa”

Comments are closed.