The House of Favourite Newspapers

Messi Akubali Kubaki Barcelona

0

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Lionel Messi, amekubali kubaki Barcelona huku akikubali pia kupunguza mshahara.

Messi sasa anajiandaa kusaini mkataba wa miaka mitano na timu hiyo ambayo ameitumikia kwa kipindi chake chote cha soka.

 

Mbali na kusaini mkataba huo, pia Messi amekubali kupunguza mshahara wake kwa asilimia 50 kutokana na hali ngumu ya kiuchumi ya timu hiyo.

 

Gazeti la ESPN, limesema kuwa mshambulaji huyo amekubali kusaini mkataba huo na kuwapiga chini Manchester City na PSG ambao walikuwa wanataka saini ya mchezaji huyo mzaliwa wa Argentina.

 

Awali mkataba wa mshambuliaji huyo, 34, alikuwa akilipwa pauni milioni 594 (trilioni 1.9) kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, lakini sasa atatakiwa kuchukua nusu ya fedha hiyo.

 

Rais wa Barcelona, Joan Laporta ameshasema kuwa anaamini kuwa mshambuliaji huyo anaweza kusaini mkataba mpya muda wowote kuanzia sasa.

Hivi karibuni La Liga, ilisema kuwa ili Barcelona wamsajili wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanapunguza gharama za mshahara wake ili wamuorodheshe kwenye listi ya wachezaji wao wapya, kutokana na bili yao ya mshahara kuvuka viwango vya kanuni za mapato na matumizi (FFP).

 

Messi alijiunga na shule ya soka ya Barcelona kwa mara ya kwanza mwaka 2000, ameshafanikiwa kucheza michezo 778 amefunga mabao 672 akiwa ametwaa makombe 10 ya La Liga, huku akitwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara nne

Leave A Reply