Messi Anyakua Ballon D’OR
Nahodha wa timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi amefanikiwa kuweka rekodi nyingine kwenye tuzo za Ballon D’OR kwa kutwaa tuzo yake ya Saba.
Nyota huyo amefanikiwa kuwashinda nyota wa Bayern Munich Robert Lewandowski na Kiungo Jorginho wa Chelsea huku mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema akiorodheshwa wa nne katika kinyang’anyiro hicho.
Messi aliisaidia timu yake ya taifa ya Argentina kutwaa uchampioni wa Copa America mwaka huu hata hivyo hii haikuwa kigezo pekee kilichomfanya ashinde tuzo hiyo bali takwimu zake kulinganisha na washindani wake kwenye tatu Bora kama zinavyoonekana kwenye picha inayofuata.