Mfanyabiashara Maarufu Nchini PCK, Aadhimisha Kifo cha Mama Yake kwa Kutoa Msaada kwa Jamii
MFANYABIASHARA maarufu nchini Patrick Christopher (PCK) katika kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya kifo cha marehemu mama yake mzazi amerudisha tabasamu kwa wanawake/ akina mama wanaojishughulisha na shughuli ya kugonga kokoto katika eneo la Tegeta Mbuyuni jijini Dar es Salaam.
Katika tukio hilo mtangazaji wa kituo cha Habari cha Global TV na 255 Global Radio Zaliam Adam anayeendesha kipindi cha Mapito alishiriki kama mwakilishi wa PCK huku kina mama hao wakisaidiwa Mchele, Maharage, Sukari, Chumvi pamoja na Pesa taslimu kwa ajili ya kuendesha Maisha yao.
PCK amefanya hivyo ikiwa ni kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha marehemu mama yake mzazi aliyefariki Septemba 30, 1996.
Katika hatua nyingine mfanyabiashara huyo kupitia mwakilishi wake Zaliam Adam ametoa kiasi cha pesa taslimu, Soda pamoja na biskuti kwa kituo cha Watoto Yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza Mori jijini Dar es Salaam.
Grace Nanyaro mmoja wa akina mama walionufaika na msaada huo wa PCK ametoa shukrani za dhati kwa mfanyabiashara huyo na kumtakia kila lakheri katika shughuli zake.