The House of Favourite Newspapers

MHE. JOKATE KUMPA SHAVU BONDIA DULLA MBABE

Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akimpongeza Bondia Dulla Mbabe,ambaye ni mzawa wa wilaya ya Kisarawe kwa ushindi alioupata dhidi ya mpinzani wake Fransis Cheka lillilofanyika hivi karibuni. 

 

SERIKALI ya wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani inatarajia kutoa eneo kwa ajili ya kujenga ukumbi utakaotumika kuwapatia mazoezi ya ngumi vijana wa wilaya hiyo.

Aidha imempongeza bondia Dulla Mbabe mzawa wa wilaya ya Kisarawe kwa ushindi alioupata dhidi ya mpinzani wake Fransis Cheka lillilofanyika hivi karibuni.

 

Hatua hiyo ya kupatiwa eneo hilo imetokana na bondia huyo kutoa kauli ya kutaka kutoa mafunzo kwa vijana wa kisarawe ili waweze kujifunza mchezo huo. Akizungumza  kuhusu mpango huo Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amesema,Mbabe amewatendea haki kwa kushinda pambano lililofanyika Desemba 26 mwaka uliopita dhidi ya Cheka.

 

Jokate alieleza, Kisarawe imejaa vipaji sio tu mpira wa miguu bali katika michezo mbalimbali. Aliahidi serikali ya wilaya kumpa uahirikiano kuhakikisha kipaji chake kinakua na kuibua vijana wengine.

 

Naye bondia huyo Mbabe alijigamba kwa kasema amecheza mipambano zaidi ya 20 ikiwemo ya kimataifa. Hata hivyo aliwaahidi watanzania kufanya vizuri katika Mchezo wa kimataifa unaokuja ambao unatarajiwa kufanyika mwezi march mwaka huu.

 

Katika hatua nyingine mbunge wa viti maalum mkoani Pwani Zainab Vullu, alimhakikishia bondia huyo, wabunge wa mkoa huo watamkaribisha Dodoma katika bunge ili kumtambulisha na kuitambulisha Kisarawe kuwa inawanamichezo lukuki sio tu wa mpira wa miguu bali na masumbwi.

Comments are closed.