The House of Favourite Newspapers

Michuano ya Kimataifa ya Kricket Kuanza Kutimua Vumbi Hapa Nchini Kesho

Mratibu wa michuano hiyo, Atif Salim.

Dar es Salaam, 1 Agosti 2024: Michuano ya Kimataifa ya Kricket ya Wavulana wa chini ya umri wa miaka 19 itaanza kutimua vumbi kesho katika Viwanja vya Gymkhana hapa jijini.

Akizungumza na wanahabari jiji leo Mratibu wa michuano hiyo Atif Salim amesema michuano hiyo itashirikisha timu kutoka mataifa manane ambayo ni Tanzania ambao ndiyo wenyeji, Malawi, Mozambique, Nigeria, Ghana, Botswana, Sierra Leon na Rwanda.

Wachezaji na viongozi wa timu shiriki wakiwa makini kusikiliza mkutano na wanahabari kuelekea michuano hiyo.

Atif amesema katika timu mbili kwenye makundi mawili yaliyogawanywa kwenye timu hizi yataingia nusu fainali na washindi kati ya hapo wanaingia fainali.

Amesema timu itakayoingia fainali itakuwa imesonga mbele na kufuzu kwenda Divisheni One kabla ya fainali ya michuano hiyo kutakuwa na mechi ya kumtafuta mshindi wa tatu ambapo mshindi huyo atakuwa ni mshindi wa mwisho wa kupata divisheni one.

Mratibu wa michuano hiyo Atif Salim (kulia) akimuuliza Nahodha wa timu ya Tanzania jinsi walivyojiandaa.

Mratibu huyo alimalizia kwa kusema fainali hiyo inatarajiwa kupigwa tarehe Agosti 11 mwaka huu ambapo pamoja na Uwanja wa Gymkhana uwanja mwingine utakaotumika ni wa Chuo Kikuu cha Mlimani (UDSM).

Msaidizi wa timu ya Tanzania, Salum Jumbe akizungumza na vyombo vya habari kuelekea michuano hiyo.

Kwa upande wake kocha Msaidizi wa timu ya Tanzania, Salum Jumbe amesema wao kama wenyeji watatumia uzoefu wa kuyazoea mazingira ikiwemo ikiwemo viwanja kuwaweza kuibuka washindi kwenye michuano hiyo.