The House of Favourite Newspapers

Miriam BSS afanyiwa kitu mbaya usiku!

    miriam-7 RICHARD BUKOS, RISASI

DAR ES SALAAM: Mwanamuziki wa Taarab, Mar­iam Mohammed Uwesu ‘Mariam BSS’ Jumapili aliyopita alijikuta akimwagiwa kojo wakati wa sherehe ya kum­bukumbu ya siku yake ya kuzaliwa ‘bethidei’ iliyofan­yika huko Manzese katika baa inayojulikana kama Bar Mpya, jirani na Friends Cor­ner Hotel.

miriam-2Katika hafla hiyo iliy­osindikizwa na Kundi la Taarab la Diamond Clas­sic Modern usiku huo, mshiriki huyo wa zamani wa shindano la kusaka vi­paji la BSS, alimwagiwa pombe, maji machafu, soda na ndoo ya chooni iliyokuwa na mikojo wakati wa tukio la kufungua shampeni, am­balo kwa desturi mpya ya sasa, mhusika humwagiwa kinywaji hicho, sambamba na maji na vinywaji vingine laini.

miriam-3Mambo yalienda vizuri hadi mshereheshaji ka­tika tukio hilo, Mc An­damakopa alipotangaza kuwa wakati wa kufun­gua shampeni umefika na mara tu baada ya kinywaji hicho kufunguli wa, wageni wa alikwa walianza kummwa­gia kwa staili ya kumuogesha.

miriam-4Kitendo hicho kiliamsha shamra kwa watu walioku­wepo, wakiwemo ‘masela’ ambao nao walimvamia na kuanza kummwagia vimim­inika mbalimbali zikiwemo pombe kali, soda na maji machafu.

miriam-5Wakati hayo yakiende­lea, wanaosadikika kuwa masela, walienda chooni na kuchukua ndoo ya maji yali­yochanganyika na mikojo na kwenda kummwagia mwilini hali iliyosababisha baadhi ya wasamaria wema kumcho­moa katikati ya kundi hilo baada ya kushtukia harufu kali ya mkojo.

miriam-6Baada ya kuchomolewa alikimbizwa chooni kwenda kuoga ndipo mambo men­gine yakaendelea huku mwanamuziki huyo akiwala­lamikia waliomfanyia kiten­do hicho akisema hakikuwa cha kiungwana.miriam-1

“Ukweli suala la kumwa­giana shampeni au maji ni la kawaida, lakini kitendo walichonifanyia cha kun­imwagia maji machafu yanayonuka harufu ya mikojo si cha kiungwana.

miriam-8“Ile ndoo wa­meitoa chooni na si unajua vyoo vya baa, walevi wengine wak­ienda kukojoa hawaangalii, wanakojolea hata maji ya kunawa , ” alilalamika Mariam.

Comments are closed.