The House of Favourite Newspapers

MJEMA: TUNAWATHAMINI BODABODA KAMA WAFANYABIASHARA WENGINE

0
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema akizungumza jambo katika hafla hiyo.

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amesema kuwa waendesha bodaboda wanathaminiwa na serikali kama walivyo wafanyabiashara wengine kwani wanaingiza kipato kupitia usafirishaji wao.

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam kwenye Viwanja vya Mashujaa alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla fupi ya vijana waendesha bodaboda wa wilaya yake waliokutana kupongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Katibu Tawala Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akifafanua jambo.

Wakielezea katika hotuba yao, waendesha bodaboda hao wamesema kuwa Rais Magufuli anapaswa kuungwa mkono na kila mwananchi kutokana na utendaji kazi wake ambao umetukuka hasa anavyozuia rasilimali za nchi zisiibiwe na watu wachache wasiopenda maendeleo ya nchi.

 

Taswira ilivyoonekana.

Katika hotuba hiyo, wameelezea mambo mengi ambayo Rais Magufuli ameyafanya kwa kipindi kifupi na hivyo kuomba waendesha bodaboda kutoka mikoa mingine kumuunga mkono kwa maendeleo yanayoonekana.

Mmoja wa wawakilishi wa waendesha bodaboda akizungumza jambo.

Akijibu hotuba hiyo, Mjema amewapongeza waendesha bodaboda akiwaeleza kuwa hotuba yao itafanyiwa kazi na serikali kwa jumla iko pamoja nao na wanachopaswa kufanya ni kuzingatia sheria za usalama barabarani.

 

Waendesha bodaboda wakiwa katika maandamano kabla ya kufika Viwanja vya Mashujaa Mnazi Mmoja, Dar.

 

Mjema amezitaka kampuni zinazofanya kazi ya kukamata bodaboda wanaoingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam, kuhakikisha wanawapatia risiti za kielektroniki ili fedha hizo ziweze kuingia katika mapato ya serikali na si vinginevyo na wazingatie sheria badala ya kuwakamata kwa kuwaonea kama wenyewe wanavyolalamika.

NA DENIS MTIMA/GPL.

Leave A Reply