Mjukuu wa Nyerere: Sioni Sura ya Babu Yangu Kwenye Ile Sanamu
MJUKUU wa Baba wa Taifa, Mwl. J. K. Nyerere, Sophia Nyerere, amesema haoni sura ya babu yake kwenye sanamu iliyochongwa na kukabidhiwa kwa Rais John Magufuli hivi karibuni katika uzinduzi wa Hifadhi mpya ya Burigi, Chato.
Amesema hayo kwenye mahojiano na Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Clouds TV.
“Kiukweli sioni sura ya babu yangu kwenye ile sanamu, aliyechora anisamehe sina nia ya kumharibia biashara, babu ameshafariki hawezi kujizungumzia ila tuliobaki tunatakiwa tuwazungumzie, nilisema ni mapema sana Watanzania kumsahau Baba wa Taifa.
“Nikiwa mdogo nyumbani walikuja wazungu walimletea zawadi ya sanamu nakumbuka babu aliikataa, haikuwa moja tu zilikuwa nyingi, kuna siku ililetwa sanamu aliniambia naionaje nikamwambia huyu ni wewe ile sanamu ipo kule nyumbani Butiama, ” amesema.
Comments are closed.