The House of Favourite Newspapers

Mke wa Mzee Yusuf Atamani Kuacha Muziki Kama Mumewe

0

 

RICHARD BUKOS | GAZETI LA AMANI| DAR ES SALAAM

MUIMBAJI wa Kundi la Jahazi Modern Taarab, Leyla Rashid, amefunguka kuwa tangu mumewe Mzee Yusuf aache kuimba Muziki wa Taarab, amekuwa hana mzuka kama zamani zaidi ya kutamani na yeye amrudie Mungu kama mumewe.

Leyla aliiambia Showbiz Xtra kuwa tangu mumewe aache kuimba na kumrudia Mungu amekuwa hana mzuka kivile wa kuimba na anatamani kumfuata mumewe ingawa bado anafikiria.

“Ukweli naimba tu lakini sina munkari kama zamani hasa baada ya mume wangu kujitoa kwenye kundi na kumrudia muumba, sijaacha rasmi kuimba ila nafikiria zaidi kumfuata mume wangu katika kumtumika Mwenyezi Mungu,” alisema.

Leave A Reply