The House of Favourite Newspapers

Mkurugenzi Mtendaji Absa Bank Tanzania Aibuka Kidedea Tuzo za Watendaji Wakuu Bora 100

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Zanzibar anayeshughulikia Masuala ya Kazi, Uchumi, na Uwekezaji, Mheshimiwa Shariff Ali Shariff, akimkabidhi Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania (wa pili kushoto), tuzo ya mshindi wa pili katika kipengele cha Mkurugenzi Mtendaji Bora wa Mwaka, katika hafla ya utoaji tuzo za Watendaji Wakuu Bora 100 wa Mwaka, jijini Dar es Salaam jana. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, ameibuka kidedea kwa kutwaa tuzo ya mshindi wa pili katika kipengele cha Mkurugenzi Mtendaji Bora wa Mwaka, katika Tuzo za Watendaji Wakuu Bora 100 wakati wa hafla ya utoaji tuzo hizo zilifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni jana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (katikati), pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo, wakipiga picha ya kumbukumbu muda baada ya mkurugenzi huyo kupokea tuzo ya Ofisa Mtendaji Mkuu Bora wa Mwaka wa Tuzo za Watendaji Bora 100 zilizoandaliwa na taasisi ya Eastern Star Consulting Group. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam jana.

Tuzo za Watendaji Wakuu Bora 100 wa Mwaka zinalenga kuwaangazia viongozi wa kipekee kutoka mashirika ya kifaida na yasiyo ya kifaida, kwa kuwatia moyo washiriki kushirikisha hadithi zao za mafanikio hivyo kuleta hamasa kwa viongozi wengine.

Tuzo hizi, zinazoratibiwa na taasisi ya Eastern Star Consulting Group, zinalenga kutambua na kusherehekea mafanikio ya kibinafsi na ya mashirika yao kupitia viongozi hao wenye utendaji uliotukuka nchini Tanzania.