The House of Favourite Newspapers

Mkuu wa Chuo Kutekwa Mwanza, MKE Asimulia, Inasikitisha – Video

KUFUATIA tukio la kutekwa kwa, Mkuu wa Chuo cha Nyakato Islamic Institute kilichopo chini ya Taasisi ya Elimu ya The Registered Trustees of Islamic, Sheikh Bashir Gora na kudai jeshi linaendelea kumtafuta, ambaye mpaka sasa ni siku nane zimepita na hajapatikana, Mke Wake Sakina, amefunguka kuhusu tukio hilo.

 

Akizungumza na Global TV, mke wa Shehe Gora ameiomba Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama kufanya jitihada za dhati ili mume wake aweze kupatikana akiwa hai kwani tukio hilo limefanya ashindwe kufanya kazi yeyote ile kutokana na mawazo ya kutunza familia ya watoto saba.

VIDEO: MSIKIE MKE WA SHEHE AKIFUNGUKA TUKIO LILIVYOKUWA

Comments are closed.