The House of Favourite Newspapers

Mkuu wa Marian Girls, Vinara Matokeo Kidato cha Nne Anena

Mkuu wa Shule ya Marian Girls, Lightness Masawe

IKIWA ni saa chache baada ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (NECTA), Dkt. Charles Msonde kutangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa 2017, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Marian Girls iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani ambao wameshika nafasi ya sita Kitaifa, Lightness Masawe amefunguka mengi kuhusu ufaulu huo.

Lightness Masawe akiwa na mtangazaji wa Global TV Online, Catherine Kahabi.

 

Akizungumza na Global Publishers, Madam Masawe amesema anamshukuru Mungu kwa ushindi huo mzuri ulioziletea heshima shule zao zote za Marian Girls na Marianm Boys.

Mandhari ya Shule ya Marian Girls.

 

Marian Girls imekuwa shule ya sita Kitaifa na kutoa mwanafunzi bora wa pili, wa tatu na wa tisa Kitaifa huku Marian Boys ikishika nafasi ya tisa Kitaifa na kutoa mwanafunzi Bora wa kwanza Kitaifa.

 

Mandhari ya Shule ya Marian Girls.

“Wanafunzi wetu tunawalea katika maadili mazuri, wanajituma kwa bidii na wanawasikiliza vyema walimu wao darasani. Kutokana na misingi yetu ya dini, watoto wetu wanakuwa watiifu na wasikivu hivyo ni rahisi kwao kutekeleza mambo yote wanayoelekezwa na walimu wao kwa ajili ya manufaa yao,” alisema Madam Masawe.

 

Orodha ya Shule 10 Bora.

1. St. Francis Girls – Mbeya
2. Feza Boys – Dar es Salaam
3. Kemoboya – Kagera
4. Bethel Sabs Girls – Iringa
5. Anwarite Girls – Kilimanjaro
6. Marian Girls – Pwani

7. Canossa – Dar

8. Feza Girls – Dar

9. Marian Boys – Pwani

10. Shamsiye Boys – Dar

 

ALICHOKISEMA MKUU WA SHULE ILIYOTOA MWANAFUNZI BORA

Global Publishers App imekurahisishia kutazama matokeo ya kidato cha nne kupitia simu ya mkononi. Install Global Publishers sasa uyasome yote: Bofya  au 

Comments are closed.