Mo Music Kwenye Ujasiriamali
STORI: GABRIEL NG’OSHA | RISASI | MIKITO NUSUNUSU
MSANII wa Bongo Fleva, Moshi Katemi ‘Mo Music’ ambaye alitamba na Wimbo wa Basi Nenda, Nitazoea, Skendo na nyinginezo amesema kwa sasa ameamua kujikita katika uzalishaji wa unga wa sembe kwa ajili ya chakula.
Akizungumza na Mikito Nusunusu, Mo Music alisema ameanzisha Kiwanda cha Katemi Food Master kwa ajili ya kuzalisha unga wa sembe na kuufunga vizuri kisha kufanya biashara kwa kusambaza sehemu mbalimbali.
“Nimeanzisha kiwanda cha Katemi Food Master ambacho kinajishughulisha na usambazaji wa unga wa sembe, kiwanda kiko kwenye kiwanja changu nilichokinunua kwetu mkoani Mwanza,” alisema Mo Music
Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam
Comments are closed.