The House of Favourite Newspapers

Mpaka Home: Haya Ndiyo Maisha Halisi ya Jacob Mbuya wa Clouds TV, Asema Hajui Kupika

jacob-mbuya-1
Makala: Imelda Mtema, Gazeti la Risasi Jumamosi, Toleo la Desemba 31, 2016

MPAKA Home inafunga mwaka leo. Inafunga na Mtangazaji na Mtayarishaji wa Kipindi cha Sports Extra cha Clouds TV, Jacob Mbuya. Yeye anaishi maeneo ya Kimara Mwisho jijini Dar. Ndani ya nyumba hiyo aliyopanga, anaishi yeye na mchumba wake ambaye kwa sasa amerudi kwao Kitunda jijini Dar kwa muda kula sikukuu.

jacob-mbuya-6Kwa wafuatiliaji wa Clouds TV, Mbuya wanamtazama kupitia kwenye habari za michezo kila siku kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, saa 1:30 hadi 2:00 usiku na Kipindi cha 360 (Alhamisi saa 3:00 asubuhi, kipengele cha michezo).

jacob-mbuya-5Mpaka Home imezungumza naye mengi hapa chini. Karibu:

jacob-mbuya-7KWA NINI MKEWE KAONDOKA?

“Si unajua tena ndiyo kwanza ametoka kujifungua, bado anapewa mawili matatu na mama mkwe. Hivyo anakuja anakaa kidogo, anarudi tena kwa mama.

jacob-mbuya-8RATIBA YAKE IKOJE NYUMBANI?

“Mimi kwa kweli si mtu wa kurudi nyumbani mapema, napenda kutazama mechi mbalimbali za ulimwenguni hivyo hapa narudi masaa machache sana kulala.

jacob-mbuya-9HUWA ANATUMIA KILEVI?

“Napiga kilevi ndiyo hususan wikiendi lakini katikati ya wiki mara nyingi huwa situmii. Mwili wangu nautengeneza ninavyotaka na ndiyo maana unaona sinenepi wala sikondi.

jacob-mbuya-10USAFI WA NYUMBA

“Huwa nafanya mimi au wakati mwingine anafanya mwenzangu. Sisi tunaishi kama marafiki, tunasaidiana hata kwenye majukumu ya usafi kama hivi unavyoona leo nafagia nyumba nzima.

jacob-mbuya-11RATIBA YAKE YA MAZOEZI

“Huwa kila siku hata niwe nimechelewa vipi kulala lakini lazima niamke saa kumi na moja alfajiri, naenda gym kisha naingia uwanjani kupasha kidogo ndiyo narudi nyumbani. jacob-mbuya-3Nikirudi, mara nyingi huwa baada ya kuoga, naanza kula matunda kisha baadaye natimka zangu kazini.

jacob-mbuya-12HANYWI CHAI?

“Daah mara nyingi huwa nakunywa kawaha ofisini kupasha tumbo moto, baada ya hapo nitakula tena mchana iwe ni wali samaki, chipsi au kitu kingine.

jacob-mbuya-13MPANGO WAKE NA SHEMEJI

“Si kwamba nimezaa naye tu ndiyo mipango imeishia hapo, hapana. Namshukuru Mungu nimeshaianza safari ya kuelekea kwenye ndoa. Nishamchumbia hivyo Mungu akipenda mwakani, tutairasimisha ndoa.

jacob-mbuya-14SARE YA KAZINI IKOJE?

“Mimi muonekano wangu nyumbani mara nyingi ni wa T-Shirt na jinzi lakini huwa nabeba suti zangu kwenye gari kwa ajili ya kutangazia si unajua huwezi kuwa na muonekano wa kiujana kwenye runinga!

jacob-mbuya-15NDOTO ZAKE

“Navutiwa sana na Kituo cha Voice of America (VOA). Ndoto  zangu siku moja ni kufanya kazi huko.

 

jacob-mbuya-16KUPIKA VEPEE?

“Kwa kweli mimi si fundi sana katike eneo hilo na mwenzangu anajua. Mfano wali sijui kupika kabisa. Kuna baadhi ya vitu ambavyo najua kama  chai, maini na mchemsho wa samaki.

jacob-mbuya-4Vingine vyote huwa naviona tu kwa mwenzangu vikiwa vishaiva. Muda wenyewe si unajua, ni nadra sana kunikuta nyumbani.

jacob-mbuya-17YUKO PEACE NA MAJIRANI?

“Yeah! Jirani wangu wa kwanza ni mama mwenye nyumba yangu. Naye anaishi hapa jirani na mimi, tunaishi vizuri na ni shabiki wangu pia. jacob-mbuya-2Anafuatilia sana vipindi vyangu vya michezo kwani naye anapenda michezo.

jacob-mbuya-18WIKIENDI HUWA INAKUWAJE?

“Mara nyingi huwa Jumamosi nawahi sana kurudi nyumbani maana huwa ratiba yangu ya Jumapili inakuwa ndefu kidogo. Naanzia kanisani misa ya pili (Kanisa Katoliki, Mashahidi wa Uganda-Magomeni), nikirudi nalala kidogo kisha nikiamka napiga msosi, naelekea Magomeni kucheza mechi maana mimi naichezea Timu ya Migration ya Magomeni ambapo kila Jumapili huwa tunakuwa na mechi.

jacob-mbuya-19SHUKRANI KWA MPAKA HOME

“Niwashukuru sana kwa kuja kunitembelea, karibuni tena siku nyingine.”

mpaka-home-jacob-mbuya-clou

Gazeti la Risasi Jumamosi, Toleo la Desemba 31, 2016

BELLE9 KIBOKO, CHEKI ALIVYOIMBA NYIMBO YAKE MPYA YA GIVE IT TO ME, SHOW YA FUNGA MWAKA ESCAPE ONE

FUNGA MWAKA: MAUA SAMA KAMA BEYONCE

Comments are closed.