Mr. Uwazi agawa zawadi kwa wasomaji wake Bagamoyo
Mr.Championi akizidi kugawa zawadi kwa wasomaji wake waliokutwa wakisoma Gazeti la Uwazi Mizengwe eneo la Stendi ya Bagamoyo.
Mr.Uwazi alipotua stendi ya Bagamoyo kugawa zawadi kwa wasomaji wake.Msomaji wa Gazeti la Uwazi Mizengwe akipozi na Mr.Uwazi huku akisoma gazeti lake kabla ya kupatiwa zawadi.
Msomaji wa Gazeti la Uwazi Mizengwe akishikilia gazeti lake kabla ya Mr.Uwazi kumpatia zawadi.Mr.Uwazi akimpatia zawadi msomaji wa Gazeti la Uwazi Mizengwe.Wadau wa Gazeti la Uwazi Mizengwe wakifurahia kutembelewa na Mr.Uwazi na kupiga naye picha.Wasomaji wa Gazeti la Uwazi Mizengwe wakiendelea kufurahia kupiga picha ya pamoja na Mr.Uwazi.Msomaji wa Gazeti la Uwazi Mizengwe eneo la Msikitini Bagamoyo akipokea zawadi yake kutoka kwa Mr.Uwazi mara baada ya kumwona akishuka kwenye gari lake.
KAMA kawaida yake Mr. Uwazi kuwajali wasomaji wake, leo ametembelea viunga mbalimbali vya maeneo ya Bagamoyo-Pwani na kuwapatia zawadi wasomaji wake waliokutwa wakilisoma kwa kuwapa zawadi mbalimbali ikiwemo sukari na kuwarudisha pesa zao walizonunulia Gazeti la Uwazi Mizengwe.
Mr. Uwazi wakati wa utoaji zawadi hizo aliambatana na ofisa usambazaji wa Global Publishers, Yohana Mkanda, ambaye wakati Mr.Uwazi akigawa zawadi hizo naye alikuwa akipokea maoni mbalimbali yanayohusu magazeti ya Uwazi Mizengwe.
Aidha Mkanda amewasihi wasomaji wa Gazeti la Uwazi kuendelea kulisoma kwani kila Mr. Uwazi atakapopita na kukuta msomaji wa gazeti hilo akilisoma atampatia zawadi papohapo.