The House of Favourite Newspapers

Mrembo Adaiwa Kutelekeza Mwanaye Kisa Mlemavu

0

mtoto-(5)Mtoto Ilham Mohamed

ARUSHA: Hujafa  hujaumbika! Mtoto Ilham Mohamed  19, (pichani) mkazi wa Ngarenaro jijini hapa amezaliwa akiwa na ulemavu wa viungo kiasi cha kumfanya aonekane mtoto mdogo, lakini bibi wa mtoto huyo, Zuleha Ismail anacholalamikia ni kitendo cha mama Ilham, Sapna Parakash kumtelekeza mwanaye.

mtoto (3)

Mtoto huyo akiwa na bibi yake, Zuleha Ismail

BIBI WA MTOTO NDIYE MWENYE KISA

Akizungumza kwa masikitiko na gazeti hili mwanzoni mwa wiki hii nyumbani kwake, Ngarenaro, bibi Ilham alisema alitelekezewa mtoto huyo mwaka 1997 na mama yake kwenda kuishi na mwanaume mwingine baada ya kuachana na mtoto wake aliyemtaja kwa jina la Mohammed Ismail.

mtoto (2)

Mrembo, Sapna Parakash

MSIKIE MWENYEWE

“Mama wa mtoto huyu amenitelekezea hapa. Aliwahi kuja mara moja lakini hakutaka kumshika wala kumbeba. Alimwambia ambariki ili apate mdogo wake kwani licha ya kutafuta tiba na mwanaume aliyenaye lakini ameshindwa kupata ujauzito.”

mtoto-(4)

 AELEZEA NDOA YA SAPNA NA MWANAYE

Bibi huyo alisema kuwa, Sapna aliolewa na mtoto wake, Mohammed ambaye aliigiza kwenye Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu.

“Baada ya kujifungua mtoto mwenye ulemavu, nahisi aliona kama laana, akaamua kumtelekeza kwangu yeye akaenda Dar. Nasikia akaolewa na mwanaume mwingine na sasa hivi yupo nje ya nchi.”

ALIKUWA NA MIEZI 3

“Aliniachia Alham akiwa na miezi 3. Sasa hivi ana miaka 19. Nimetumia fedha nyingi kumtibu maradhi aliyonayo. Ana mtindio wa ubongo uliosababisha miguu kukosa nguvu ya kusimama, mgongo kupinda na shingo kuzunguka bila mpangilio.”

MATIBABU YAKE NI INDIA

“Niliwahi kumpeleka hospitali moja ya hapa Arusha, daktari bingwa wa magonjwa hayo akaniambia, Ilham anatakiwa kwenda kufanyiwa upasuaji nchini India. Kwa hiyo niandae kiasi cha shilingi milioni 24.

“Nimekuwa nikitumia shilingi 50,000 kila wiki kumnunulia dawa. Kwa kipindi chote hadi kufikia leo hii, nimeshatumia pesa nyingi na sasa hivi sina kitu jamani,” alisema bibi huyo.

Amani lilimpigia simu baba wa mtoto huyo, Mohammed ambaye alisema: “Ni kweli Ilham ni mwanangu. Mama yake sijui hata alipo. Mimi hali yangu kipesa ni mbaya, sina kitu.”

mtoto (1)

ALIYEGUSWA NA HABARI

Kwa mwenye kuguswa na habari ya bibi Ilham na anataka kunmsaidia mtoto huyo anaweza kuwasiliana naye kwa kutumia namba; 0754568378 au 0622300250.

Leave A Reply