Mrembo amtibu Aunt kitambi
Mrembo Fatina Deus, ‘Fettylicious’ akiwa na Aunt Ezekiel.
Imelda Mtema
MREMBO aliyejulikana kwa jina la Fatina Deus, ‘Fettylicious’ amesema amempa bure tiba ya kitambi staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ili kumuondolea kero aliyokuwa akiipata.
Akipiga stori na gazeti hili, Fettylicious alisema miongoni mwa watu waliokuwa wakisumbuka na tatizo la kuwa na kitambi ni Aunt lakini kwa kuwa yeye lengo lake ni kuwasaidia mastaa wengi, amempa Aunt bure dawa hiyo ili wengine wamtafute.
“Nimempa dawa ya asili kabisa ya kuondoa tumbo ambalo ni kero kwa warembo wengi, Aunt atapona na ninawashauri na mastaa wengine wanione ili waondokane na aibu ya kuwa na matumbo utadhani wajawazito,” alisema Fettylicious.