Mrundi: Kisinda Ataibeba Yanga
KOCHA Mkuu wa Aigle Noir ya Burundi, Gustave Niyonkuru, amevutiwa na kiwango kilichooneshwa na kiungo mshambuliaji mpya wa Yanga, Mkongomani, Tuisila Kisinda.
Kauli ya kocha huyo imekuja baada ya kumshuhudia Kisinda akifunga bao na kucheza kwa kiwango cha juu katika mechi ya kirafiki walipokutana wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.
Niyonkuru alisema:“Nimevutiwa na yule aliyekuwa akishambulia kutokea pembeni na kufanikiwa kufunga bao la kwanza, wanamwita Kisinda, ni mchezaji mzuri na kwa kweli atawasaidia sana Yanga.
STORI: JOEL THOMAS