Msemaji wa Serikali, Polepole Wafunguka Ajali ya Lori Moro
MKURUGENZI wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbas, na Msemaji wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole, leo Agosti 10, 2019, wametoa kauli zao kupitia akaunti zao za Twitter, kuhusiana tukio la lori lenye kubeba mafuta kupinduka mjini Morogoro eneo la Msamvu na baadaye kulipuka na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 60 na kujeruhi 70.
Wengi wa waliofariki ni wale waliokuwa wakichota mafuta kutoka katika lori hilo.
Katika akaunti yake huo, Dkt. Abbas amesema:
”Tumepokea kwa masikitiko taarifa kuhusu ajali ya lori la mafuta, Morogoro, iliyosababisha moto na kuunguza watu kadhaa. Mkuu wa Mkoa na timu za uokoaji wanaendelea kukabiliana na hali katika eneo la tukio. Taarifa kamili kuhusu idadi ya vifo na majeruhi itatolewa badae. Tunaendelea kutoa wito kwa wananchi kukaa mbali na eneo la ajali hasa yanapohusika magari au vyombo vingine vya usafiri vilivyobeba vitu vinavyoweza kuripuka kama mafuta.”.
Comments are closed.