The House of Favourite Newspapers

Mshindi wa Milioni 100 za Vodacom M-Pawa Akabidhiwa Kitita Chache

   mwanza2

Pichani ni Bi. Paulina Kulwa (Kulia) akikabidhiwa hundi ya mfano wa Tsh Milioni 100 baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na M-Pawa.

Hapa kazi tu ni kauli mbiu inayohamasisha watu kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia fursa mbalimbali zilizopo, usemi huu umetimia kwa Mama Paulina Kulwa mkazi wa Mwanza baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni mia moja kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya CBA.

Paulina alikabidhiwa hundi hiyo katika ofisi za Vodacom jijini Mwanza na Meneja Masoko na huduma za Kifedha Vodacom Tanzania, Noel Mazoya na kusema lengo la kuanzisha huduma hii ni kuwasaidia Watanzania kuwa na utamaduni wa kuweka akiba.

Aidha, Bi. Kulwa baada ya kukabidhiwa hundi alisema “Namshukuru Mungu na Vodacom kuanzisha huduma hii maana tayari imenifanya kuwa milionea na kuanzisha ajira kwa Watanzania wengine, lakini pia watoto wangu wanaenda shule na nina nyumba”

yanga
Bi Paulina Kulwa (Kulia) akiwa na pacha wake katika duka la Vodacom City Mall jijini Mwanza katika hafla ya kumpongeza na kumkabidhi hundi baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na M-Pawa.

Naye Mkuu wa kitengo cha masoko Benki ya CBA, Solomon Kawishe alishukuru ushirikiano kati ya Benki yake na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kuleta neema kwa Watanzania.

mwanza3

Mshindi wa Jiongeze na Mpawa akiwa na maafisa toka Vodacom na CBA katika hafla fupi ya kumkabidhi mfano wa hundi na kumpongeza. Toka kushoto ni Ayubu Kalufya Mkuu wa Vodacom Kanda ya Ziwa, Meneja Masoko wa huduma za Kifedha wa Vodacom Noel Mazoya, mshindi wa milioni 100 Bi Paulina Kulwa, Solomoni Kawishe Mkuu wa Masoko – CBA na Eric Luyangi Mkuu wa MPawa – CBA.

Comments are closed.