The House of Favourite Newspapers

Msondo Wafunika Leaders Club

0

1.Waimbaji wa Bendi ya Msondo Ngoma wakionesha ujanja wao kwa mashabiki.

Waimbaji wa Msondo Ngoma wakionesha ujanja wao kwa mashabiki.

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma jana ilifunika vilivyo katika tamasha kubwa la kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika kampeni ya kuchangia madawati mashuleni.

Tamasha hilo lilifanyika jana usiku katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar ambapo sehemu ya mapato ya tamasha hilo yatatumika kununulia madawati.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makonda alisema serikali itaendelea kutoa sapoti kubwa kwa wanamuziki wa dansi ili kuuendeleza na kuuboresha muziki huo ili ufike mbali kama ilivyokuwa siku za nyuma.

Miongoni mwa bendi zilizotoa burudani kwenye tamasha hilo ni Msondo Ngoma, Mlimani Park, Yamoto, QS International na nyingine nyingi.

 

2.Msondo Ngoma wakitoa burudani.

Msondo Ngoma wakitoa burudani.

3.Wapiga gitaa wa Bendi ya Msondo Ngoma katika ubora wao.

Wapiga gitaa wa Msondo Ngoma katika ubora wao.

4.Bendi ya Sikinde akitoa burudani.

Mlimani Park wakitoa burudani.

5.Sikinde wakiendelea kutoa burudani

Mlimani wakiendelea kutoa burudani.

6.Mwimbaji wa bendi ya QS International akiimba kwa hisia kali.

Mwimbaji wa bendi ya QS International akiimba kwa hisia kali.

7.QS wakiendelea kutoa burudani.

QS wakiendeleza makamuzi.

8.Mpiga ngoma wa Msondo Ngoma akionesha utundu wake.

Mpiga ngoma wa Msondo Ngoma akionesha utundu wake.

9. Msondo wakiendelea kutoa burudani.

Msondo wakiendelea kutoa burudani.

10. Wanamuziki wa Yamoto Bendi wakitoa burudani.

Wanamuziki wa Ya Moto Bendi wakitoa burudani.

11.Yamoto Bendi wakiendelea kutoa burudani.

Ya Moto Bendi wakiendelea kutoa burudani.

12.Yamoto Bendi ikizidi kuwaburudisha mashabiki.

Ya Moto Bendi ikizidi kuwaburudisha mashabiki.

13.Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda akizungumza jambo mbele ya wanamuziki hao (hawapo pichani).

Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda akizungumza jambo mbele ya wanamuziki hao (hawapo pichani).

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply