The House of Favourite Newspapers

Msuva Amzima Kichuya, Yanga Yafunga Mabao 35

kichuya

Kiungo mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya.

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam, Championi Jumatano Toleo la Januari 4, 2017

YANGA juzi ilifanikiwa kufungua mwaka kwa kishindo zaidi baada ya kuichapa timu ya Jamhuri ya Pemba kwa mabao 6-0 kwenye mchezo wa Kombe la Mapinduzi.

championi-1

Huu ulikuwa muendelezo wa Yanga wa kupachika mabao mengi kwenye michezo yake ambayo imecheza kuanzia Agosti, mwaka jana, lakini kikiwa ndiyo kichapo kikubwa zaidi wamekitoa kuanza kipindi hicho.

Mbali na Yanga, Simba nao wamekuwa wakikutana na baadhi ya timu na kuzipa dozi kubwa ambapo leo Championi linachambua ni mchezaji gani kinara wa kupachika mabao pale timu hizo zinapofunga kuanza mabao matatu na kuendelea kwenye mchezo mmoja.

yanga-4

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva (kulia) akishangilia na wachezaji wenzake.

Katika idadi hiyo ya mabao kuanzia msimu huu ulipoanza mwezi Agosti, Yanga wanaonekana kuwa kidedea kwa kutoa dozi nene zaidi baada ya kushinda michezo tisa kwa mabao matatu au zaidi huku Simba wao wakishinda michezo minne tu kwa mabao matatu au zaidi, ambayo ni nusu ya ile ya Yanga.

Msuva..1.jpg

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva.

Katika uchambuzi huo, kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva ameonekana kuteka nchi baada ya kuwa kinara wa kupachika mabao kwenye michezo hiyo huku akimwacha mbali kiungo mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya.

Yanga katika michezo hiyo tisa ambayo wameshinda kwa idadi hiyo ya mabao, Msuva amefanikiwa kufunga mabao nane, huku timu jumla ikifunga mabao 35.

Msuva ambaye kwa jumla kwenye ligi ana mabao tisa, anaonekana kuwa kwenye michezo hiyo mingi alikuwa akifunga mabao mawili-mawili.

Wakati Yanga walipoichapa JKT Ruvu mabao 3-0, yeye alifanikiwa kupachika mawili, pia mchezo wa juzi dhidi ya Jamhuri alifunga mawili.

Mabao mengine alifunga kwenye mchezo dhidi ya African Lyon waliposhinda mabao 3-0, ambapo alifunga bao moja, dhidi ya Mtibwa Sugar walishinda 3-1 yeye akafunga bao moja, Kagera Sugar walishinda mabao 6-2 ambapo alifunga bao moja, lakini pia kwenye mchezo wa pili dhidi ya JKT Ruvu alifunga bao moja.

simba-sc

Kikosi cha timu ya  Simba.

Mchezaji wa Yanga anayemfuatia Msuva kwa kupachika mabao kwenye michezo hiyo ni Donald Ngoma, ambaye ana mabao saba akifuatiwa na Amissi Tambwe ambaye ana mabao sita, huku Obrey Chirwa akiwa na manne, Deus Kaseke ana matatu, Vincent Bossou na Juma Mahadhi wana mawili kila mmoja na Kamusoko ana moja.

Wakati Simba wenyewe wakiwa ndiyo vinara kwenye Ligi Kuu Bara huku Kichuya akiwa ameshafunga mabao tisa, kwenye michezo minne ambayo timu yake ilishinda kuanzia mabao matatu na kuendelea yeye amefanikiwa kuwa kinara kwa kupachika mabao manne tu, yakiwa ni nusu ya yale ya Msuva.

Simba ambao msimu huu wamekuwa wakishinda kwa mabao 2-0, 2-1 au 1-0 mara nyingi, walifanikiwa kupata ushindi mnono kwenye mchezo dhidi ya Majimaji ambapo walishinda kwa mabao 4-0 na Kichuya akafanikiwa kupachika mawili.

Huu ndiyo ulikuwa mchezo wao waliotoa dozi kubwa zaidi, mingine ambayo wameshinda kwa ushindi mkubwa ni dhidi ya Ndanda, Toto African na Mwadui, yote hiyo wameibuka na ushindi wa mabao 3-0.

Jamal Mnyate, ambaye amefungana na Mzamiru Yassin, Laudit Mavugo pamoja na Mohamed Ibrahim kila mmoja akiwa amefunga mabao mawili, hawa wanaonekana kuachwa mbali sana na mshindi wa pili wa Yanga.

Hawa wameachwa na Ngoma kwa mabao matano na ukiunganisha mabao yao yote kwa pamoja, wanafikisha nane ambayo ndiyo yanakuwa sawa na ya Msuva.

Hakika hata kama Yanga hawatatwaa makombe msimu huu lakini watakuwa wamegawa dozi za hatari kwa wapinzani na ni dhahiri wana safu kali ya ushambuliaji msimu huu.

Matokeo makubwa ya Yanga

Yanga  3-0  African Lyon

Kaseke

Msuva

Mahadhi

Yanga3-0  Majimaji

Kaseke

Tambwe

Tambwe

Yanga  3-1 Mtibwa Sugar           

Chirwa                                 

Msuva

Ngoma

Kagera Sugar 2-6  Yanga

Donald Ngoma

Simon Msuva

Obrey Chirwa

Deus Kaseke

Obrey Chirwa

Donald Ngoma   

Yanga   4-0  JKT Ruvu                

Obrey Chirwa

Amissi Tambwe

Simon Msuva

Amissi Tambwe

Yanga   3-0   Mbao

Bossou

Emmanuel Mseja (OG)

Tambwe

JKT Ruvu  0-3  Yanga

Michael Aidan (jifunga)

Msuva

Msuva

Yanga  4-0  Ndanda

Amissi Tambwe

Donald Ngoma*2

Vincent Bossou

Yanga  6-0  Jamhuri

Msuva *2

Ngoma *2

Mahadhi

Kamusoko

Matokeo makubwa Simba

Simba    3-1   Ndanda

Laudit Mavugo

Frederic Blagnon

Shiza Kichuya

Simba    4-0  Majimaji

Mnyate

Kichuya

Mnyate

Kichuya

 

Simba    3-0   Toto African

Mzamiru Yasin

Laudit Mavugo

Mzamiru Yasin

Mwadui FC  0-3   Simba

Mohammed Ibrahim

Kichuya

Mohammed Ibrahim

 halotel-strip-1-1

Waone Wolper na Harmonize Wakidendeka Live Jukwaani

Comments are closed.