Staa wa Bongo Muvi, Sabrina Omary.
Stori: Imelda Mtema, Wikienda
Dar es Salaam: Makubwa! Mtoto wa staa wa Bongo Muvi, Sabrina Omary aitwaye Ashfaq amemtoa nishai mama’ke huyo baada ya kumtwanga swali la Kiingereza na alipochelewa kumjibu alimwambia kuwa staa anatakiwa kujibu swali kwa haraka.
Tukio hilo lilijiri kwenye duka moja la nguo ndani ya Mlimani City, Dar baada ya mtoto huyo kumuuliza kwa Kiingereza nini maana ya neno ‘majestic’ ndipo msanii huyo akawa anajing’atang’ata.