The House of Favourite Newspapers

Mtoto Kumpa Mamilioni Wolper

0

BAADA ya kupigiwa vigelegele vya uzazi, sasa mtoto kumpa msanii Jacqueline Wolper mamilioni.
Wolper mwenyewe anacheeeka alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa makampuni mawili makubwa ambayo yanataka kumpa mwanaye aitwaye P mkataba wa ubalozi wenye thamani ya mamilioni ya fedha.

 

Kwa wenye udaku wao mji huu ni mdogo, ujumbe wa uhakika umeanika wazi kuwa huwenda dili hilo la mtoto wa Wolper likakamilika kabla ya Juni 21, mwaka.

 

“Kuna mipango inanibana kuhusu mtoto wangu, nadhani nitakuwa huru kuanzia tarehe 23 mwezi huu,” alisema Wolper alipoulizwa na paparazi wetu kuhusu kuwepo kwa taarifa za mwanaye kulamba ubalozi.

 

Kama jambo hilo litatimia msanii huyo ataweza kujipatia kitita kikubwa cha fedha kutokana na malipo atakayopewa mwanaye aliyezaa na mwanaume aitwaye Rich Mitindo.

Leave A Reply