The House of Favourite Newspapers

Mtoto Yatima Yamkuta Mazito, Inasikitisha

0

 

Abuu Hussein

 

KIBAHA: Siku chache tangu kupita kwa Siku ya Mtoto wa Afrika, mwanafunzi wa darasa la tano, Abuu Hussein (11) wa Shule ya Msingi Miembe Saba wilayani Kibaha, mkoani Pwani ambaye ni yatima yamemkuta mazito kufuatia ku­sumbuliwa na vidonda mguuni.

Kutokana na hali hiyo, yuko hatarini kupata ulemavu endapo hatapata matibabu ya haraka.

Akizungumza na gazeti hili nyumbani kwa bibi yake huko Miembe Saba, mwanafunzi huyo alisema ana miezi mitatu ameshindwa kwenda shuleni kutokana na maumivu makali yanayomkabili yaliyosababish­wa na vidonda.

Hussein ambaye ni yatima akiishi na bibi yake, Tatu Kiumbo (65) alipata tatizo hilo miezi mi­tatu iliyopita alipokuwa akicheza mpira na wenzake na kuanza kusikia maumivu kwenye mguu wake wa kulia.

 

“Yalianza maumivu mgu­uni na bibi alifikiri labda nimeu­mizwa na wenzangu, hali iliyo­mfanya anikande lakini maumivu yaliendelea kwa siku kadhaa na baadaye ilitokea kama kajipu, lakini kalikuwa kanauma sana,” alisema Hussein.

Aliendelea kusema kuwa bibi yake alimpeleka hospitali ambayo ni Kituo cha Afya cha Mkoani ambacho kwa sasa kimepandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya, alitibiwa na kuandikiwa dawa za kunywa pamoja na kupaka.

“Baada ya kupasuliwa siku chache baadaye vikatokea vi­donda vingine vingi ambavyo vilikuwa vikitoa maji na mguu ukaanza kuvimba na kusababi­sha nishindwe hata kusimama,” alisema Hussein.

Bibi wa yatima huyo, Tatu al­isema kuwa mjukuu wake kwa sasa haendi hospitali baada ya kuambiwa awe anatumia dawa kwa kunywa na kupaka baada ya kusafisha vidonda kila siku ambapo kwa sasa ana zaidi ya wiki tatu anatibiwa nyumbani.

Tatu alisema kuwa mjukuu wake amekuwa akipata mau­mivu makali usiku ambapo in­ambidi kumpa dawa za kutuliza maumivu.

“Kwa sasa wote tunauguzana kwani na mimi nashindwa kum­hudumia vizuri, nami naumwa presha ambayo imenisaba­bishia kushindwa hata kutem­bea huku muda mwingi nikiwa nimelala tu, naomba watu wa­tusaidie maana hali yetu ni mbaya,” alisema Tatu.

 

Alisema kuwa hana msaada wowote kwani anaishi na wa­toto wa ndugu zake ambao nao hawana kazi ya aina yoyote, maisha yao yakitegemea mis­aada ya majirani.

Kwa upande wake mjomba wa mwanafunzi huyo, Idd Miki­dadi ambaye amekuwa akim­peleka hospitali na kumrudisha, alisema angalau kwa sasa ame­pata nafuu kwani alikuwa hawezi hata kusimama na mguu ulikuwa ukitoa maji .

Mikidadi alisema kuwa kama kuna msaada wa kumsaidia mto­to huyo ili apate matibabu zaidi itakuwa ni vizuri kwani anateseka na kwa sasa hata masomo ames­imama kutokana na tatizo hilo.

Akizungumzia tatizo hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Miembe Saba, Hamis Shomary alisema kuwa baada ya kupata taarifa hizo walikwenda na kamati ya serikali ya mtaa kumuona mtoto huyo na kuweka mpango wa kumpeleka hospitali kwa matibabu zaidi.

Shomary alisema kuwa tatizo kubwa kwenye familia hiyo ni uw­ezo ndiyo umesababisha mtoto huyo asipate matibabu ya uhak­ika na kusababisha mguu wake kuzidi kuwa kwenye hali mbaya.

Naye Katibu wa Kamati ya Mtaa kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, Mwana­hamis Saadi alisema kutokana na tatizo hilo, watahakikisha wa­nashirikiana na wadau ili mtoto huyo apatiwe matibabu ya kina.

Saadi alisema kuwa hata kama itatokea wadau wameshindwa kumchangia, watajitolea wao na kamati ya mtaa ili kuhakikisha Abuu anapata matibabu ili arejee shuleni na ndoto zake ziweze ku­timia.

Aliyeguswa na tatizo la mwa­nafunzi huyo, awasiliane na bibi yake kwa namba 0718 56 95 77.

MWANDISHI WETU | RISASI MCHANGANYIKO

 

 Breaking News: CUF ya Lipumba Yatangaza Kumaliza Mgogoro Wao, Wamtaka Maalim Seif na Wenzake Warudi

Leave A Reply